Lissu kuendelea kusota rumande kwa zaidi ya siku 90, shauri lake likisogezwa mbele 

July 15, 2025 6:28 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Upande wa Jamhuri waomba shauri liahirishwe kuipa muda Mahakama Kuu kutolea majibu maombi yao.

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tundu Lissu ataendelea kusota mahabusu kwa zaidi ya siku 90 sasa, mara baada ya shauri la uhaini namba 8607/2025 linalomkabili kuahirishwa mpaka Julai 30.

Shauri hilo limeahirishwa kufuatia upande wa Jamhuri kuomba kesi iahirishwe baada ya wao kupeleka maombi Mahakama Kuu ya kutaka mashahidi katika kesi hiyo watoe ushahidi kwa kificho kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kulinda usalama wao.

Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu Franco Kiswaga aliridhia ombi hilo na kueleza kuwa sababu ya kuahirishwa kesi iliyotolewa na upande wa Jamhuri ina mashiko.

Tundu Lissu ataendelea kusota mahabusu kwa zaidi ya siku 90 sasa, mara baada ya shauri la uhaini namba 8607/2025 linalomkabili kuahirishwa mpaka Julai 30. Picha | DW

Maombi ya upande wa Jamhuri ambayo yaliwasilishwa kwa mujibu wa Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai yamepingwa na mshtakiwa Lissu kwa kudai kuwa hakuna sababu ya msingi kwa upande wa Jamhuri kupewa ahirisho jingine. 

“Walitakiwa wapeleke kwanza hiyo taarifa Mahakama Kuu, haizuii hayo maombi walioomba. Kwanini hawajapeleka taarifa Mahakama Kuu?, kwa sababu wanacheza na Mahakama yako, kwa sababu unawaruhusu,” amehoji mshtakiwa Lissu mahakamani hapo.

Mbali na pingamizi la ahirisho la shauri linalomkabili, Lissu aliwasilisha ombi jingine la kuiomba Mahakama kutumia Mamlaka ya Msingi ya Kuzaliwa nayo (Inherent Power) kumfutia mashataka na kumuacha huru.

Hata hivyo, Hakimu Kiswaga ameeleza kuwa, mahakama hiyo haiwezi kutumia Mamlaka ya Msingi ya Kuzaliwa nayo kwa sababu shauri hilo lipo katika hatua ya kupelekwa Mahakama Kuu (Committing stage) na sio hatua ya usikilizwaji (Listening stage).

Lissu aliwasilisha ombi la kuiomba Mahakama kutumia Mamlaka ya Msingi ya Kuzaliwa nayo (Inherent Power) kumfutia mashataka na kumuacha huru. Picha | IPP Media

Mbali na maamuzi yaliyotolewa, Mahakama imeutaka upande wa Jamhuri kutotumia nafasi iliyotolewa na Mahakama kuchelewesha uendeshwaji wa shauri hilo na kuwataka kushughulikia maombi waliyopeleka Mahakama Kuu kwa uharaka.

Lissu anatimiza siku 97 tangu alipokamatwa na Jeshi la Polisi Aprili 9, 2025 alipokuwa katika mkutano wa kisiasa wa chama chake mkoani Ruvuma.

Kwa mara ya kwanza Lissu alifikishwa mahakamani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam Aprili 10, 2025 ambapo shauri linalomkabili litaendelea kusikilizwa.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Nukta TV

Sakata bei ya mafuta kupanda latua BoT, Naibu Gavana atoa ufafanuzi

Sakata bei ya mafuta kupanda latua BoT, Naibu Gavana atoa ufafanuzi

Nukta TV

BoT yabakiza Riba ya Benki Kuu 5.75% kudhibiti mfumuko wa bei

BoT yabakiza Riba ya Benki Kuu 5.75% kudhibiti mfumuko wa bei

Nukta TV