Waziri Mkuu Mstaafu Cleopa David Msuya afariki dunia

May 7, 2025 6:23 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  • Rais Samia atangaza bendera kupepea nusu mlingoti kwa siku saba za maombolezo.
  • Taarifa zaidi kuhusu msiba zitaendelea kutolewa na serikali.

Dar es Salaam. Waziri Mkuu mstaafu wa Tanzania Cleopa David Msuya amefariki dunia leo katika Hospitali ya Mzena, Dar es Salaam alipokuwa anapatiwa matibabu ya maradhi ya moyo.

Taarifa ya kifo cha Msuya imetangazwa leo majira ya alasiri na Rais Samia aliyebainisha kuwa kiongozi huyo amefariki majira ya saa 3 asubuhi leo Mei 07, 2025 katika Hospitali ya Mzena, jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa moyo.

“Hayati Cleopa David Msuya ameugua kwa muda mrefu na amekuwa akipatiwa matibabu ndani na nje ya nchi ikiwemo katika Hospitali ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Hospitali ya Mzena na kule jijini London,’’ amesema Rais Samia

Aidha, Rais Samia ametuma salamu zake za pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na Watanzania wote kwa msiba na kutangaza siku saba za maombolezo ambapo bendera zitapepea nusu mlingoti kuanzia Mei 07 hadi 13 mwaka huu.

“Taarifa zaidi kuhusu msiba huu zitaendelea kutolewa na serikali, poleni sana Watanzania,” ameeleza kwa masikitiko Rais Samia.

Marehemu Msuya alizaliwa Januari 4,1931 huko Chomvu Usangi, Wilaya ya Mwanga, mkoa wa Kilimanjaro ambapo alisoma Chuo Kikuu cha Makerere kati ya 1952–1955 na kisha kufanya kazi za maendeleo vijijini hadi 1964. 

Cleopa David Msuya katika picha enzi za uhai wake. Picha/ Global publisher.

Kuanzia mwaka huo alihudumu kama Katibu Mkuu katika wizara mbalimbali hadi 1972, alipoteuliwa kuwa Waziri wa Fedha na baadaye kushika nyadhifa mbalimbali ikiwa ni pamoja na Waziri wa Viwanda, Waziri Mkuu (1980–1983 na tena 1994–1995), na Waziri wa Fedha na Mipango hadi 1994. Baada ya uchaguzi wa 1995 alibaki kuwa Mbunge hadi alipostaafu mwaka 2000. 

Hata baada ya kustaafu, aliendelea kushiriki katika siasa kupitia CCM na alikuwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Maendeleo la Kilimanjaro. Mnamo Oktoba 23, 2019 aliteuliwa kuwa Mkuu wa Chuo cha Ardhi akiwa na umri wa miaka 88.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV