Serikali yawataka watendaji kuongeza kasi ya ukusanyaji mapato

September 25, 2019 7:00 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Wametakiwa kuhakikisha suala la ukusanyaji wa mapato linapewa kipaumbele katika maeneo yao.
  • Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema bila mapato ya uhakika, miradi ya maendeleo haitatekelezwa kwa wakati.

Dar es Salaam. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amewataka watendaji wa Serikali kuongeza kasi ya ukusanyaji mapato kwani ujenzi wa miradi ya maendeleo zikiwemo shule na hospitali haiwezi kutekelezwa bila mapato ya uhakika.

Amesisitiza kuwa watendaji wahakikishe suala la ukusanyaji wa mapato linapewa kipaumbele katika maeneo yao ikiwemo ukusanyaji wa kodi na tuzo mbalimbali.

“Ukusanyaji wa mapato ni muhimu kwa ajili ya maendeleo ya Taifa kwa sababu miradi ya maendeleo kama ujenzi wa shule haiwezi kutekelezeka bila ya kukusanya mapato,” amesema Majaliwa jana (Septemba 24, 2019) wakati akipokea taarifa ya mkoa wa Iringa alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Iringa kwa ajili ya ziara ya kikazi.

Katika hatua nyingine amesema mahusiano kati ya Serikali na wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa kidini, kimila ni muhimu yakaimarishwa.


Zinazohusiana: 


Kwa mujibu wa taarifa ya Ofisi ya Waziri Mkuu, ni lazima mahusiano hayo yakadumishwa katika ngazi zote kwa sababu Serikali ipo kwa ajili ya wananchi wote na inawahudumia bila ya ubaguzi.

Amewataka viongozi waliopewa dhamana ya kusimamia maeneo mbalimbali nchini wahakikishe wanatekeleza majukumu yao ipasavyo na uwajibikaji wao uwe na tija.

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Ally Hapi amesema mkoa huo umepewa zaidi ya Sh7 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa hospitali za Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Kilolo na Mufindi.

Mkuu huyo wa mkoa amesema mbali na fedha hizo za ujenzi wa hospitali pia Serikali imetoa zaidi ya Sh3 bilioni kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa vituo vya afya.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
16 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Nukta TV

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Nukta TV

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV