Wakulima wahimizwa kuongeza uzalishaji wa mazao msimu wa mvua za vuli

November 27, 2019 8:49 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Mvua hizo za vuli ambazo huanza Oktoba hadi Desemba ni mahususi kwa maeneo ya nchi yanayopata vipindi viwili vya mvua kwa mwaka ambapo hujumuisha mikoa ya Kanda ya Ziwa Victoria, Ukanda wa Pwani ya Kaskazini na Nyanda za juu Kaskazini Mashariki. 
  • Wakulima wakumbushwa kupanda mazao yanayokomaa muda mfupi. 

Dar es Salaam. Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga amewataka wakulima katika mikoa inayopata mvua mara mbili kwa mwaka, kutumia vizuri mvua za vuli zinazoendelea kunyesha kuzalisha mazao yanayokomaa kwa muda mfupi ili kujipatia kipato kutokana na kilimo hicho.

Taarifa iliyotolewa leo (Novemba 27, 2019) na Wizara ya Kilimo, inaeleza kuwa mvua hizo tayari zimeanza kunyesha katika mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Mara, Simiyu, Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Pwani na Morogoro na zikitumiwa vizuri zitaleta manufaa makubwa.

“Wakulima wanahamasishwa kutumia vizuri mvua hizi kwa kupanda kwa wakati,” anasema Hasunga katika taarifa hiyo.

 Aidha, Waziri Hasunga amewaagiza Wakuu wa Wilaya kuwasimamia Maafisa Ugani Kilimo ili waweze kuwasaidia wakulima kuzingatia kanuni bora za kilimo kwa kupanda mbegu bora kulingana na kanda za kiekolojia na kutumia mbolea inayostahili kwenye mazingira husika.

Wizara ya Kilimo imesema itaendelea kutoa ushauri wa kitaalam na maelekezo kwa wakulima na wananchi nchini kuhusu mwenendo wa mvua na hatua za kuchukua ili kuhakikisha kunakuwa na uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara ya kutosha na hatimaye nchi kuwa na usalama wa chakula.



Mvua hizo za vuli ambazo huanza Oktoba hadi Desemba ni mahususi kwa maeneo ya nchi yanayopata vipindi viwili vya mvua kwa mwaka ambapo hujumuisha mikoa ya Kanda ya Ziwa Victoria, Ukanda wa Pwani ya Kaskazini na Nyanda za juu Kaskazini Mashariki. 

Septemba 3, 2019, Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) ilitoa mwelekeo wa msimu za vuli za Oktoba hadi Desemba ambapo ilisema mvua katika kanda hizo tatu utatofautiana na hivyo tahadhari na mambo ya kufanya yanaweza kutofautiana.

Kuwepo kwa tofauti ya mvua kunasababishwa na mifumo ya hali hewa hasa joto la bahari na mvumo wa upepo kuelekea nchi kavu.

Hata hivyo, TMA ilieleza kuwa wananchi wanapaswa kujiandaa na kutumia vizuri mvua hizo kwa sababu zitakuwa za kutosha. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
26 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
26 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
26 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Elimu ya kodi mwarobaini wa wafanyabiashara kuikwepa TRA, ianzie shuleni

Elimu ya kodi mwarobaini wa wafanyabiashara kuikwepa TRA, ianzie shuleni

Nukta TV

Rais Samia: Serikali chini ya Magufuli haikutaka kuyumbishwa kukamili kwa JNHPP

Rais Samia: Serikali chini ya Magufuli haikutaka kuyumbishwa kukamili kwa JNHPP

Nukta TV

Rais Samia: Umeme wa SGR hautoingiliwa, Dodoma umeme uhakika 24/7

Rais Samia: Umeme wa SGR hautoingiliwa, Dodoma umeme uhakika 24/7

Nukta TV