Serikali yawataka wahisani kuangazia changamoto za ubunifu Tanzania

March 9, 2020 12:51 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Wahisani watakiwa kuwekeza fedha kwa wabunifu wenye mawazo yanayotatua changamoto za jamii. 
  • Wadau wa ubunifu wamewasisitiza wabunifu kufikia changamoto za vijijini na siyo kubaki mjini pekee.
  • Hata hivyo, ubunifu isikaririke kuwa ni lazima utumie teknolojia.

Dar es Salaam. Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wiliam Ole Nasha amewataka washirika wa maendeleo kuwekeza fedha kwa wabunifu wa teknolojia wenye mawazo yanayotekelezeka ambayo yanatatua changamoto za msingi zinazoikabilia Tanzania. 

Olenasha aliyekuwa akizungumza leo (Machi 9, 2020) katika uzinduzi wa Wiki Ya Ubunifu kwa mwaka 2020 jijini Dar es Salaam amesema hali hiyo imekuwa changamoto katika kukuza ubunifu Tanzania kwa sababu wabunifu hawafikiwi katika kiwango kinachohitajika. 

Amesema hata wabunifu wanaosaidiwa wengi wao ni wale ambao bidhaa ziko kwenye wazo bado hazijaenda sokoni, jambo linalochukua muda mrefu kutoa suluhisho la changamoto za jami.

“Tumefikia wabunifu wangapi? Nimesikia humu ndani wabunifu wote wanajuana, ni wale wale.Tunaweza kuwa tunarundikana kutoa uhisani kwa mbunifu mmoja. Wabunifu wapo wengi huko nje,” amesema Ole Nasha. 

Amesema ni vema wigo wa ubunifu Tanzania ukapanuliwa kuhahakikisha vijana wengi wenye mawazo ya kibunifu wanasaidiwa kuendeleza kazi zao ili kuwarahisishia maisha Watanzania kwa teknolojia rahisi.  

Wiki ya Ubunifu (#IW2020) imeandaliwa na Mfuko wa Ubunifu wa Maendeleo ya Watu (HDIF) kwa kushirikiana na washirika wa maendeleo ikiwemo Tume Ya Sayansi na Teknolojia (Costech), Seedspace Dar es Salaam na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Uingereza (DFID).

Pia ni jukwaa muhimu kwa wabunifu kuonyesha kazi zao hasa suluhisho za teknolojia zinazogusa sekta mbalimbali ili kuboresha maisha ya watu na kuifanya Tanzania kuwa sehemu nzuri ya kuishi.


Soma zaidi:


Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania, Hisham Hendi akizungumza katika uzinduzi huo amesema changamoto nyingine ni kuwa wabunifu wengi wanakwama kwasababu wanashindwa kuangalia changamoto za moja kwa moja zinazowakabili Watanzania. 

Akitolea mfano wa M-Pesa, Hendi amesema sababu za mfumo huo kufanikiwa ni kuwa uliangazia shida ambayo watu walikuwa nayo na siyo watu wa mjini tu hata wa vijijini.

Wadau mbalimbali wa ubunifu wamekubaliana na njia moja ambayo imeonekana kujirudia kwenye vinywa vyao ambayo ni kumulika kwa karibu changamoto halisi za wananchi na kuzitafutia suluhisho la teknolojia la kudumu. 

 Mwakilishi Mkaazi wa Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Christina Musisi amesema ubinifu sasa unatambulika kama suluhisho kwa changamoto ambazo zinaikumba jamii na ili kuuweka ubunifu katika nafasi hiyo, wabunidu na wavumbuzi hawana budi kuangazia changamoto ambazo ni kiini cha maisha duni ya wananchi.

Amesema suluhisho za teknolojia ni muhimu zilenge kutengeneza fursa za ajira kwa vijana ili kuboresha maisha yao.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV