Bei ya viazi mviringo haikamatiki Mtwara

September 14, 2020 12:05 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Bei inayotumika leo Mtwara ni zaidi ya mara mbili ya bei ya Iringa na Dar es Salaam, jambo linalowafaidisha zaidi wafanyabiashara ambao wamepeleka viazi mviringo mkoani humo. 
  • Gunia la kilo 100 la viazi mviringo katika masoko ya mkoa wa Mtwara  linauzwa kwa Sh110,000, wakati masoko ya  Iringa na Dar es Salaam linauzwa kwa Sh45,000.

Dar es Salaam. Watumiaji wa viazi mviringo hasa kutengeneza chipsi katika Mkoa wa Mtwara leo watalala na maumivu kutokana na bei ya gunia la kilo 100 la zao hilo kuuzwa zaidi ya mara mbili ya bei inayotumika katika Mikoa ya Iringa na Dar es Salaam na Njombe. 

Takwimu za mazao makuu ya chakula zilizotolewa na Wizara ya Viwanda na Biashara  leo (Septemba 14, 2020) zinaeleza kuwa gunia la kilo 100 la viazi mviringo katika masoko ya mkoani Mtwara linauzwa kwa Sh110,000, wakati masoko ya Njombe na Dar es Salaam linauzwa kwa Sh45,000.

Hiyo ina maana kuwa bei inayotumika leo Mtwara ni zaidi ya mara mbili ya Iringa na Dar es Salaam, jambo linalowafaidisha zaidi wafanyabiashara ambao wamepeleka viazi mviringo mkoani humo. 

Bei hiyo inayotumika Mtwara ndiyo bei ya juu huku ya Iringa na Dar es Salaam ikiwa ni ya chini ikilinganishwa na bei zinazotumika katika maeneo mengine nchini.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
30 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
30 May, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
AKILI UNDE INAVYOIMARISHA HUDUMA ZA AFYA YA KINYWA NA MENO

AKILI UNDE INAVYOIMARISHA HUDUMA ZA AFYA YA KINYWA NA MENO

Nukta TV

WAFAHAMU 'THE BIG FIVE' WA AFRIKA

WAFAHAMU 'THE BIG FIVE' WA AFRIKA

Nukta TV

HIVI NDIVYO UNAWEZA KUSAFISHA MENO YAKO

HIVI NDIVYO UNAWEZA KUSAFISHA MENO YAKO

Nukta TV