Serikali yafuta maonyesho ya nane nane mwaka 2021

February 10, 2021 11:24 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Sherehe hizo zilizokuwa zifanyike mwezi Agosti, 2021 katika kanda nane katika mikoa 26 ya Tanzania Bara.
  • Fedha zilizotengwa kwa ajili shughuli hiyo zitatumika kuimarisha huduma za ugani ili kuleta mapinduzi ya kilimo. 
  • Serikali kufanya tathmini ya ufanisi ya maonyesho hayo miaka ijayo. 

Dar es Salaam. Waziri wa Kilimo Prof Adolf Mkenda ametangaza kufutwa kwa sherehe za maonyesho ya wakulima maarufu kama Nane Nane kwa mwaka 2021 na fedha zilizotengwa kwa ajili shughuli hiyo zitatumika kuimarisha sekta ya kilimo.  

Sherehe hizo zilitakuwa zifanyike mwezi Agosti, 2021 katika kanda nane katika mikoa 26 ya Tanzania Bara.

Prof Mkenda amesema Serikali inakusudia fedha zote za umma zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya maadhimisho ya sherehe hizo zitumike kuimarisha huduma za ugani nchini.

“Shughuli zote za Nanenane mwaka huu zimefutwa rasmi na Serikali. Hhivyo fedha zote zilizotengwa kwa kazi hiyo zitatumika kuboresha huduma za ugani nchini ili kuleta mapinduzi ya kilimo,” amesema waziri huyo leo (Februari 10, 2021) Jijini Dodoma mbele ya  waandishi wa habari.

Amesema shughuli za Nane Nane lazima ziendane na upatikanaji wa huduma bora za ugani kuinua sekta ya kilimo, hivyo Serikali lazima ijipange vema.


Zinahusiana: 


Kufuatia uamuzi huo wa Serikali, Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na wadau itatumia muda huo kufanya tathmini ya namna maonyesho ya Nane Nane yamekuwa yakifanyika na kuona maeneo ya kuboresha  ili yawe na tija katika kukuza sekta ya kilimo na kuchangia ukuaji wa uchumi wa Taifa kwa ujumla. 

Aidha, Prof Mkenda amesema wizara yake itaunda kikosi kazi maalum kwa ajili ya kufanya tathmini hiyo ili kilete mapendekezo yatakayokuwa na tija katika maadhimisho ya Nane Nane katika miaka ijayo.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Rais Samia: AFCON ni fursa, wawekezaji karibuni kuwekeza

Nukta TV

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Utani wa Rais Samia, matokeo kati ya Simba na Yanga

Nukta TV

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Rais Samia awataka wananchi wa Kizimkazi kutunza miundombinu ya maji

Nukta TV