Dhana potofu zinawazuia baadhi ya watu kujikinga na Corona

March 6, 2021 9:35 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni pamoja na kuamini kuwa watoto hawawezi kupata Corona na kuwa kuvaa barakoa kunasababisha ukosefuwa hewa.

Dar es Salaam. Ugonjwa wa Corona ni kati ya masuala mtambuka kwa mataifa mengi duniani huku ukiacha majeraha ya moyo baada ya wapendwa wa baadhi ya watu kupoteza maisha.

Hata hivyo, vifo vinavyotokana na ugonjwa wa Corona bado siyo fundisho kwa baadhi ya watu kwani wengine wameendelea kupuuzia kanuni za kujikinga na ugonjwa huo na hivyo kusababisha kuongezeka kwa maambukizi na idadi ya vifo vinavyotokana na ugonjwa huo. 

Hivi karibuni, Mkurugenzi wa huduma za dharura wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dk Michael Ryan alisema, licha ya mataifa mengi kuweka juhudi za kukabiliana na Corona ikiwemo kufunga mipaka na kutoa chanjo, Corona inaweza isitokomezwe lkabisa mwaka huu.

Dk Ryan ameyasema hayo wakati akizungumza na vyombo vya habari Jijini Geneva nchini Uswisi huku akikiri kushangazwa na kuongezeka kwa idadi ya maambukizi katika nchi mbalimbali zikiwemo Marekani, nchi za Ulaya na Asia.

“Tunafanya kazi zaidi kuelewa hali ya kuongezeka kwa maambukizi. Mengine ni kwa sababu ya kulega kwa kuzingatiwa kwa kanuni za afya ya jamii na watu kuacha kuchukua tahadhari,” amesema Dk Ryan.

Je, ni dhana zipi ambazo huenda zikawa sababu ya kuendelea kuongezeka kwa maambukizi ya Corona? Tazama video hii kujifunza zaidi.

                          

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV