Utarajie nini ukipata chanjo ya Corona?

August 2, 2021 11:50 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Unaweza kupata changamoto za afya za muda mfupi.
  • Ni pamoja na maumivu ya kichwa na kichefu chefu.

Dar es Salaam. Chanjo dhidi ya ugonjwa wa Corona inatolewa kwa ajili ya kumsaidia mtu kukabiliana na ugonjwa huo pale atakapoupata kwa sababu inaongeza kinga ya mwili dhidi mashambulizi ya virusi. 

Kwa sasa, Tanzania imeanza kutumia chanjo aina ya Johnson & Johnson ambapo inatolewa katika vituo 550 mikoa yote. 

Kwa mujibu wa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Dorothy Gwajima, mnamo Julai 28, 2021 wakati wa uzinduzi wa chanjo hiyo,  imesaidia nchi zilizoendelea ikiwemo Marekani na Uingereza katika kupunguza vifo vya watu pamoja na idadi ya watu wanaolazwa hospitalini na kuwekewa gesi ya oksijeni.

Dk Gwajima alisema, kuna taarifa nyingi za uongo kuhusiana na chanjo ya Uviko-19 ikiwemo watu kupata changamoto za kiafya baada ya kupata ikiwemo vifo.

Hata hivyo, waziri huyo alisema, ni kawaida kwa watu kupata changamoto ndogo ndogo ikiwemo kuumwa kichwa baada ya baada ya kupata chanjo lakini hazidumu muda mrefu.

Unataka kujifunza kuhusu changamoto hizo ambazo ni za kawaida? Tazama video hii:

                       

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW