Heslb kutoa majina waliopata mikopo awamu ya pili Oktoba 21

October 18, 2021 8:48 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Waliopata awamu ya kwanza ni 37,731.
  • Majina awamu ya pili kutolewa ndani ya siku tatu.
  • Wanafunzi 70,000 wa mwaka kwanza kupata mikopo.

Dar es Salaam. Baada ya wanafunzi 37,731 wa mwaka wa kwanza kupata mikopo elimu ya juu kwa mwaka 2021/22, Serikali inatarajia kutoa awamu ya pili ya orodha ya majina mengine Oktoba 21 mwaka huu. 

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza idadi ya wanafunzi hao Oktoba 17, 2021 ambapo mikopo yao thamani yao in Sh99.9 bilioni.

Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul-Razaq Badru amesema kuwa kati ya wanafunzi hao (37,731), wanaume ni 23,379 sawa na asilimia 62.

Badru amesema kuwa HESLB imeanza kupeleka fedha za wanafunzi waliopangiwa mikopo katika vyuo mbalimbali na kuwataka wanafunzi kupata taarifa za kina katika akaunti walizotumia kuomba mkopo maarufu kama SIPA (Student’s Individual Permanent Account) na kujiandaa kwenda vyuoni kwa ajili ya kujisajili.

“Serikali imeshatupatia fedha na tumeanza kuzipeleka vyuoni…lengo letu ni kuhakikisha wanafunzi wanaopangiwa wanazikuta fedha vyuoni ambako watajisajili na kupokea ili watimize ndoto zao,” amesema Badru.

Kuhusu kutangazwa kwa orodha ya awamu ya pili, Badru amesema imepangwa kutolewa Alhamisi, Oktoba 21, 2021 baada ya kukamilisha uchambuzi wa maombi unaoendelea na kuwataka waombaji mikopo kutembelea akaunti zao ya SIPA kupata taarifa kuhusu maombi yao.

“Orodha hii ya kwanza inajumuisha wanafunzi wenye sifa zikiwemo kuwa wahitaji, wameomba kwa usahihi na wana udahili wa chuo kimoja… tunakamilisha uchambuzi wa maombi mengine na tutaoa orodha ya pili katika siku mbili zijazo,” amesema Badru.

Aidha, Bodi imewataka waombaji wa mikopo kuwa watulivu wakati mchakato wa upangaji wa mikopo kwa wanafunzi wenye sifa kwa awamu inayofuata ukiendelea.

Serikali imetenga Sh570 bilioni kwa ajili ya mikopo kwa wanafunzi 160,000. Kati yao, wanafunzi 70,000 watakuwa ni wanufaika wapya na wanafunzi zaidi ya 90,000 ni wale wanaoendelea na masomo baada ya kufaulu mitihani yao ya mwaka. 

Hadi kufikia Septemba 30, HESLB ilikuwa imepokea maombi 88,688 na huenda asilimia 12 ya walioomba wanaweza wasipate mikopo hiyo kwa sababu ya bajeti iliyopo kutokidhi mahitaji ya waombaji wote.

Mikopo hiyo husaidia wanafunzi kuweza kumudu gharama za masomo na maisha wakati akisaka elimu hiyo ya juu. 

Wangapi watatoboa awamu ya pili ya HESLB? Usikose kufuatilia habari za HESLB katika tovuti ya www.nukta.co.tz na mitandao yake.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
27 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
27 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
27 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Wizara tano zilizoidhinishiwa fedha nyingi 2026-27

Wizara tano zilizoidhinishiwa fedha nyingi 2026-27

Nukta TV

Waziri Khamis: Serikali haijaongeza kodi kwa bodaboda

Waziri Khamis: Serikali haijaongeza kodi kwa bodaboda

Nukta TV

Nyavu za samaki zamuibua Ado Shaibu bungeni, Spika Zungu amtuliza

Nyavu za samaki zamuibua Ado Shaibu bungeni, Spika Zungu amtuliza

Nukta TV