Majaliwa atoa maagizo mazito pikipiki za maafisa ugani

June 8, 2022 11:09 am · David
Share
Tweet
Copy Link
  • Aagiza pikipiki zilizopo wizarani wapewe maafisa hao.

Dar es Salaam. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametoa siku kwa Wizara ya Kilimo iwe imeondoa pikipiki zote katika ofisi za wizara hiyo zilizopo jijini Dodoma na kuzikabidhi kwa wakurugenzi wa halmashauri nchini.

Majaliwa aliyekuwa akikagua Ofisi za Wizara ya Kilimo zilizopo eneo la VETA, Dodoma na kukuta pikipiki zilizotolewa kwa ajili ya maafisa ugani zikiendelea kuwepo, amesema kuanzia leo Juni 8, 2022 hadi Juni 12, 2022 pikipiki hizo ziwe zimeondolewa kwa sababu zimekaa muda mrefu. 

“Hii haikubaliki, Wakurugenzi wote waandikiwe barua waje wazichukue, kama kuna ufungaji wa plate number utafanyika huko huko. Jumapili saa 10 jioni ziwe zimefika kwa wahusuka,” amesema Majaliwa.

Aprili 4, 2022, Rais Samia Suluhu Hassan alizindua ugawaji wa vitendea kazi vilivyoandaliwa na Wizara ya Kilimo kwa ajili ya maafisa ugani wote nchini. Vifaa ni pamoja na pikipiki.

Amesema tayari Rais Samia alishazikabidhi kwa ajili ya kupelekwa kwa maafisa ugani, hivyo kitendo cha pikipiki hizo kuendelea kubaki katika eneo hilo hakikubaliki.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Profesa Siza Tumbo amemuhakikishia Waziri Mkuu kwamba wamepokea maelezo hayo na watayafanyia kazi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
16 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Nukta TV

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Nukta TV

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV