15 washikiliwa, msako wenye magari namba SSH 2530

September 4, 2025 6:27 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Muliro asisitiza kuwa kutumia namba hizo ni kosa kisheria

Dar es salaam. Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia watu 15 kwa tuhuma za kuendesha magari yenye namba SSH 2530, kinyume na sheria. Hatua hiyo ni mwendelezo wa operesheni ya kuhakikisha maagizo yaliyotolewa awali kuhusu marufuku ya namba hizo yanatekelezwa ipasavyo.

Akizungumza leo Alhamisi, Septemba 4, 2025, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, amesema watuhumiwa tayari wamekamatwa huku msako dhidi ya wengine ukiendelea.

“Mtu yeyote anayebandika namba hizo, baada ya kufuatiliwa kwenye mifumo ya usajili wa namba, hili ni kosa kisheria,” amesema Muliro.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, amesema watuhumiwa tayari wamekamatwa huku msako dhidi ya wengine ukiendelea. Picha | Mwananchi.

Kwa mujibu wa Muliro, watu hao wamekamatwa kwa mujibu wa Kifungu cha 13(1) cha Sheria ya Usalama Barabarani, Sura ya 168 Marejeo ya 1973 yaliyorekebishwa mwaka 2023, ambayo inaeleza kuwa ni kosa la jinai kwa mtu yeyote kuendesha chombo cha moto bila namba halali za usajili na yeyote anayekiuka hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

“Tunaendelea kusisitiza kuwa ni makosa na suala hili ni kinyume cha sheria kwa sababu namba hizo hazipo,” amesisitiza Muliro.

Itakumbukwa kuwa Agosti mwaka huu, Jeshi la Polisi Tanzania kupitia Msemaji wake, David Misime, lilitangaza marufuku ya matumizi ya namba hizo na kuwataka wamiliki wa magari kuondoa ifikapo Septemba 1, 2025. 

Kutoka kwa marufuku ya Jeshi la Polisi kumekuja hiyo mara baada ya vyombo mbalimbali vya moto kuonekana vikitumia namba hiyo hivi karibuni jambo lililozua mijadala hususan katika majukwa mbalimbali ya mitandao ya kijamiii huku wengine wakihusisha utumiaji wa namba hizo na siasa katika kipindi kampeni kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.