Zungu achaguliwa kuwa Spika mpya Tanzania

November 11, 2025 1:16 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni baaada ya kupata kupigiwa kura na wabunge kwa asilimia 98.6.

Arusha. Aliyekuwa Naibu Spika wa Bunge la Tanzania Mussa Azzan Zungu kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM) amechaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Tanzania baada ya kupata kura 378 kati ya kura 383 zilizopigwa.

Zungu ambaye ni mbunge  wa jimbo la Ilala amewamwaga wagombea wengine waliokuwa wanawania nafasi hiyo kwa kupata asilimia 98.6 ya kura zote zilizopigwa.

Zungu alikuwa akichuana na wagombea wengine akiwemo Veronica Charles Tyeah kutoka Chama cha National Reconstruction Alliance (NRA),

Anitha Alfan Mgaya kutoka Chama cha National League for Democracy (NLD) na Chrisant Nyakitita kutoka Chama cha Democratic Party (DP).

Wengine ni Ndonge Said Ndonge kutoka Chama cha Alliance for Africa Farms Party (AAFP) na Amin Alfred Yango kutoka Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC).

Uchaguzi huo umefanyika leo Novemba 11, 2025 jijini Dodoma na kuongozwa na Mwenyekiti wa uchaguzi, Mbunge wa Jimbo la Isimani, William Lukuvi ambaye amepitishwa na wabunge kuongoza uchaguzi huo.

Kwa ushindi huo, Zungu anachukua nafasi ya Dk Tulia Ackson aliyehudumu katika nafasi hiyo kwa miaka mitatu tangu mwaka 2022 baada ya aliyekuwa Spika wa Bunge wa wakati huo Job Agustino Ndugai kujiuzuru Januari 6, 2022.

Aahidi ushirikiano kwa wabunge, Serikali

Baada ya kutangazwa mshindi Zungu amewashukuru wabunge kwa muchagua huku akihidi kutoa ushirikiano kwa wabunge hao pamoja na Serikali kwa ajili ya ustawi wa Tanzania.

“Niwahakikishie kuwa ushindi huu ni wetu sote, hamjanichagua ili niongoze Bunge lakini mmenichagua niwatumikie na kuhakikisha yale yote tuliyokubaliana kama vipaumbele vya Taifa kwa kipindi cha miaka mitano ijayo yanafanikiwa…

…Naahidi kutoa ushirikiano kwa Serikali kwamba kama Bunge tuntashauri na kutoa maazimio ya Bunge kwa ajili ya ustawi wa wananchi na maendeleo endelevu kwa ustawi wa nchi yetu,” amesema Zungu.

Pamoja na hayo, Zungu amemshukuru mtangulizi wake Dk Tulia Ackson kwa kumpa mafunzo na maelekezo yaliyomjenga na kumuimarisha akiahidi kuyaendeleza kwa wasaidizi wake watakaochaguliwa akiwemo Naibu Spika.

“Ninaaahidi viongozi watakao chaguliwa kuwa wasaidizi wangu, Naibu Spika na baadae Wenyekiti wa Bunge,  tutashirikiana kuongoza Bunge hili la 13 kwa kutoa maamuzi ya haki na kuzingatia uadilifu…

…Hakutakuwa na upendeleo wowote tutaongoza kwa kufuata katiba sheria za nchi na kanuni za Bunge kwa vyama vyote vyenye uwakilishi bungeni,” ameongeza Zungu.

Zungu ambaye amekuwa mbunge kwa miaka 20 anakuwa Spika wa nane atakayeliongoza Bunge hilo la 13 kwa miaka mitano ijayo.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
7 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
7 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV