Zanzibar yafikisha wagonjwa 24 wa Corona

April 16, 2020 10:51 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Serikali imetangaza wagonjwa wapya sita leo na kufikisha idadi ya wagonjwa 24 visiwani humo. 
  • Wagonjwa hao wapya, watano ni wanaume na mmoja ni mwanamke.

Dar es Salaam. Idadi ya wagonjwa wa virusi vya corona (COVID-19) Zanzibar  imezidi kuongezeka na kufikia 24 baada ya Wizara ya Afya visiwani humo kutangaza wagonjwa wapya sita.

Waziri wa Afya wa Zanzibar, Hamad Rashid Mohammed katika taarifa yake iliyotolewa leo (Aprili 16, 2020) amesema wagonjwa wote ni Watanzania na hawana historia ya kusafiri nje ya nchi siku za hivi karibuni. 

“Wagonjwa wote wamelazwa katika vituo maalum kwa ajili ya kuendelea na matibabu,” amesema Mohammed. 

Idadi ya wagonjwa hao wapya inafanya Zanzibar kushika nafasi ya pili kwa wagonjwa wengi wa COVID-19 baada ya Dar es Salaam ambayo hadi kufikia jana (Aprili 15,2020) ilikuwa na wagonjwa 62 katika ya 88 walioripotiwa.

Akizungumzia wagonjwa hao wapya, Mohammed amesema wagonjwa watano ni wanaume na mmoja ni mwanamke ambao wote ni wakazi wa Zanzibar.

Mgonjwa wa kwanza ni mwanaume mwenye miaka 30 mkazi wa Kibweni, wa pili mwanaume (27) mkazi wa Magogoni huku watatu pia ni mwanaume mwenye miaka 28 anaishi Kwarara. 


Zinazohusiana:


Wengine ni mwanamke (58) anayeishi Kilamahewa Juu, wa tano ni mwanaume (23) mkazi wa Amani na mwisho ana miaka 55 ambaye ni mwanaume anayeishi Kidoti visiwani humo. 

Aidha, waziri huyo amewataka wananchi wanaofiwa na ndugu zao kuchukua tahadhari za afya hasa wanapowazika maiti na ikiwezekana washirikiane na wataalam wa afya. 

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imewaomba wananchi kuendelea kuchukua tahadhari kwa kunawa mikono mara kwa mara, kuepuka kugusa pua, mdomo au macho, kutumia tishu wakati wa kukohoa au kupiga chafya.

Pia wanakumbushwa kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima hasa katika masoko na vituo vya daladala na watu wenye dalili za ugonjwa huo wametakiwa kufika katika vituo vya afya ili wafanyiwe uchunguzi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV