Zanzibar yafikisha wagonjwa 24 wa Corona

April 16, 2020 10:51 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Serikali imetangaza wagonjwa wapya sita leo na kufikisha idadi ya wagonjwa 24 visiwani humo. 
  • Wagonjwa hao wapya, watano ni wanaume na mmoja ni mwanamke.

Dar es Salaam. Idadi ya wagonjwa wa virusi vya corona (COVID-19) Zanzibar  imezidi kuongezeka na kufikia 24 baada ya Wizara ya Afya visiwani humo kutangaza wagonjwa wapya sita.

Waziri wa Afya wa Zanzibar, Hamad Rashid Mohammed katika taarifa yake iliyotolewa leo (Aprili 16, 2020) amesema wagonjwa wote ni Watanzania na hawana historia ya kusafiri nje ya nchi siku za hivi karibuni. 

“Wagonjwa wote wamelazwa katika vituo maalum kwa ajili ya kuendelea na matibabu,” amesema Mohammed. 

Idadi ya wagonjwa hao wapya inafanya Zanzibar kushika nafasi ya pili kwa wagonjwa wengi wa COVID-19 baada ya Dar es Salaam ambayo hadi kufikia jana (Aprili 15,2020) ilikuwa na wagonjwa 62 katika ya 88 walioripotiwa.

Akizungumzia wagonjwa hao wapya, Mohammed amesema wagonjwa watano ni wanaume na mmoja ni mwanamke ambao wote ni wakazi wa Zanzibar.

Mgonjwa wa kwanza ni mwanaume mwenye miaka 30 mkazi wa Kibweni, wa pili mwanaume (27) mkazi wa Magogoni huku watatu pia ni mwanaume mwenye miaka 28 anaishi Kwarara. 


Zinazohusiana:


Wengine ni mwanamke (58) anayeishi Kilamahewa Juu, wa tano ni mwanaume (23) mkazi wa Amani na mwisho ana miaka 55 ambaye ni mwanaume anayeishi Kidoti visiwani humo. 

Aidha, waziri huyo amewataka wananchi wanaofiwa na ndugu zao kuchukua tahadhari za afya hasa wanapowazika maiti na ikiwezekana washirikiane na wataalam wa afya. 

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imewaomba wananchi kuendelea kuchukua tahadhari kwa kunawa mikono mara kwa mara, kuepuka kugusa pua, mdomo au macho, kutumia tishu wakati wa kukohoa au kupiga chafya.

Pia wanakumbushwa kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima hasa katika masoko na vituo vya daladala na watu wenye dalili za ugonjwa huo wametakiwa kufika katika vituo vya afya ili wafanyiwe uchunguzi.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.