Wiki yaisha kwa machungu Soko la Hisa Dar

February 29, 2020 10:24 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Thamani ya mauzo ya wiki nzima imeshuka kwa takriban asilimia tatu hadi Sh18.7 bilioni kutoka Sh19.3 milioni iliyorekodiwa juma lililopita.
  • Wachambuzi waeleza kuwa licha kushuka kwa thamani ya mauzo, matumaini ya kufanya vizuri katika soko hilo bado yapo.

Dar es Salaam. Thamani ya mauzo ya wiki nzima katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) imeshuka kidogo kwa takriban asilimia tatu hadi Sh18.7 bilioni kutoka Sh19.3 milioni iliyorekodiwa juma lililopita huku wachambuzi wakitabiri mwenendo chanya siku zijazo.

Uchambuzi wa soko kwa wiki iliyoanzia Februari 21 hadi 28, 2020 uliofanywa na kampuni ya udalali ya masoko ya mitaji na dhamana, Zan Securities, unabainisha kuwa thamani ya mauzo katika soko hilo ulishuka  kwa asilimia 2.6 kutoka yale ya wiki iliyopita.

Wiki za DSE hujumuisha siku za kazi pekee yaani Jumatatu hadi Ijumaa.


Soma zaidi: Thamani ya mauzo soko la hisa Dar yapaa zaidi ya mara 40


“Licha ya kushuka thamani ya mauzo, bado soko linatoa matumaini ya kufanya vizuri siku zijazo kwa sababu kiasi na mauzo ya jumla ya wiki yako  thabiti katika viwango vya mabilioni,” imesema taarifa iliyotolewa leo (Februari 29, 2020) na Mtendaji Mkuu wa Zan Securities, Raphael Masumbuko.

Wakati thamani ya mauzo ya jumla ya DSE ikishuka, benki ya NMB imechangia asilimia 94 ya thamani mauzo yote ya wiki iliyoishia Februari 28.

NMB imefuatiwa kwa mbali na kampuni ya bia Tanzania (TBL) ambayo imechangia asilimia 2.9 na benki ya CRDB kwa asilimia 2.85.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.