Wawekezaji wa Acacia soko la hisa Dar tabasamu tupu

May 14, 2019 4:14 pm · Nuzulack Dausen
Share
Tweet
Copy Link
  • Wawekezaji wa kampuni hiyo ya madini leo wamevuna Sh100 zaidi kwa kila hisa kutoka bei ya jana.
  • Wenzao wa CRDB ni miongoni mwa waliopoteza zaidi leo.

Dar es Salaam. Wawekezaji wa kampuni ya Acacia (ACA) katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) leo watalala na tabasamu baada ya thamani ya hisa za kampuni hiyo kupanda kwa asilimia 2.25 na kuwafanya waweke kibindoni Sh100 zaidi kwa kila hisa moja kutoka kiwango cha jana Mei 13, 2019.

Ripoti ya soko ya siku ya DSE ya Mei 14 inaonyesha kuwa hadi soko linafungwa thamani ya hisa moja ya Acacia ilikuwa ni Sh4, 550 kutoka Sh4,450 iliyorekodiwa jana.

Hata wakati wawekezaji wa Acacia wakinehemeka leo, wenzao wa CRDB watalala na maumivu baada ya thamani ya hisa za benki hiyo kushuka kutoka Sh130 kwa hisa moja iliyorekodiwa jana wakati soko linafungwa hadi Sh120 leo hii jioni. 


Zinazohusiana: M-pesa, intaneti vyachangia Vodacom Tanzania kupata faida ya Sh90 bilioni


Licha ya thamani za hisa za CRDB kushuka, bado ndiyo kampuni iliyoongoza kwa kuuza kiwango kikubwa cha hisa sokoni leo.

Kampuni nyingine ambazo thamani ya hisa zake imeshuka leo ni Shirika la Ndege la Kenya (KA) kwa asilimia 5.88, Kampuni ya Habari ya NMG (asilimia 2.34) na Kampuni ya bia ya East African Breweries Ltd (EABL).

Acacia ndiyo kampuni iliyofanya vizuri zaidi leo sokoni huku nyingi zikibaki katika viwango vilivyokuwepo jana zikiwemo Vodacom, na TICL licha ya kutangaza mwenendo mzuri wa kimapato wa kampuni zao hivi karibuni.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV