Wawekezaji wa Acacia soko la hisa Dar tabasamu tupu

May 14, 2019 4:14 pm · Nuzulack Dausen
Share
Tweet
Copy Link
  • Wawekezaji wa kampuni hiyo ya madini leo wamevuna Sh100 zaidi kwa kila hisa kutoka bei ya jana.
  • Wenzao wa CRDB ni miongoni mwa waliopoteza zaidi leo.

Dar es Salaam. Wawekezaji wa kampuni ya Acacia (ACA) katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) leo watalala na tabasamu baada ya thamani ya hisa za kampuni hiyo kupanda kwa asilimia 2.25 na kuwafanya waweke kibindoni Sh100 zaidi kwa kila hisa moja kutoka kiwango cha jana Mei 13, 2019.

Ripoti ya soko ya siku ya DSE ya Mei 14 inaonyesha kuwa hadi soko linafungwa thamani ya hisa moja ya Acacia ilikuwa ni Sh4, 550 kutoka Sh4,450 iliyorekodiwa jana.

Hata wakati wawekezaji wa Acacia wakinehemeka leo, wenzao wa CRDB watalala na maumivu baada ya thamani ya hisa za benki hiyo kushuka kutoka Sh130 kwa hisa moja iliyorekodiwa jana wakati soko linafungwa hadi Sh120 leo hii jioni. 


Zinazohusiana: M-pesa, intaneti vyachangia Vodacom Tanzania kupata faida ya Sh90 bilioni


Licha ya thamani za hisa za CRDB kushuka, bado ndiyo kampuni iliyoongoza kwa kuuza kiwango kikubwa cha hisa sokoni leo.

Kampuni nyingine ambazo thamani ya hisa zake imeshuka leo ni Shirika la Ndege la Kenya (KA) kwa asilimia 5.88, Kampuni ya Habari ya NMG (asilimia 2.34) na Kampuni ya bia ya East African Breweries Ltd (EABL).

Acacia ndiyo kampuni iliyofanya vizuri zaidi leo sokoni huku nyingi zikibaki katika viwango vilivyokuwepo jana zikiwemo Vodacom, na TICL licha ya kutangaza mwenendo mzuri wa kimapato wa kampuni zao hivi karibuni.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.