Wasiofuata vitambulisho vya Nida kikaangoni

January 17, 2025 1:31 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Nida yasema itawasitishia matumizi ya namba ya utambulisho wa Taifa.

Arusha. Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida) imetangaza kusitisha matumizi ya namba ya utambulisho wa Taifa (NIN) kwa Watanzania watakaoshindwa kuchukua vitambulisho vyao kwa wakati.

Taarifa ya James Kadi, Mkurugenzi Mkuu wa Nida iliyotolewa leo Januari 17, 2025 inabainisha kuwa watakaofungiwa matumizi ya namba hizo ni wale ambao watashindwa kuvifuata vitambulisho vyao mwezi mmoja baada ya kutumiwa ujumbe mfupi (sms) na mamlaka hiyo.

“Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa inawatangazia wale wote ambao hawajajitokeza kuchukua vitambulisho vyao na watakaopokea ujumbe mfupi wa maandishi katika simu zao (sms), kufika katika ofisi za NIDA za wilaya walikojisajili kuchukua vitambulisho vyao kama itakavyoelezwa katika ujumbe huo…

… Atakayeshindwa kufanya hivyo matumizi ya Namba ya Utambulisho wake wa Taifa (NIN) yatasitishwa baada ya mwezi mmoja tangu kupokea ujumbe huo,” imesema taarifa ya Kadi.

Taarifa ya Nida inakuja ikiwa umesalia mwezi mmoja kutekeleza agizo la Waziri wa Mambo ya Ndani Innocent Bashungwa aliyeitaka mamlaka hiyo kugawa vitambulisho milioni 1.2 ndani ya miezi miwili.

Waziri Bashungwa alitoa agizo hilo Disemba 17, 2024 katika ziara ya kikazi katika mamlaka hiyo jijini Dar es Salaam, ambapo pia aliwataka kupunguza urasimu unaokwamisha ufanikiwaji wa zoezi hilo nchini.

Nida imetoa taarifa hiyo baada ya jitihada za kuwafikia wananchi wenye vitambulisho vilivyokamilika kupitia ofisi za watendaji wa Kata, Vijiji, Mitaa Vitongoji na Shehia kugonga mwamba.

Zoezi hilo lililofanyika Oktoba 12, 2023 hadi Machi 2024 lillilenga kuongeza upatikanaji wa vitambulisho hivyo kwa Wananchi baada ya umuhimu wake kuongezeka katika shughuli mbalimbali ikiwemo za kijamii.

Ikiwa matumizi hayo ya namba yatasitishwa kuna baadhi ya Wananchi watakosa huduma muhimu ikiwemo kusajili laini za simu, kujiunga na huduma za kibenki, kuomba kazi katika mifumo rasmi ya serikali, kupokea vipeto na vifurushi pamoja na huduma nyingine nyingi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
13 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV