Wanunuzi wa kahawa waonywa Kagera

June 10, 2020 7:30 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Watakiwa kufuata bei elekezi ya Sh1,200 kwa kilo.
  • Pia watakiwa kufanya biashara hiyo mchana kweupe bila kuwahujumu wakulima.
  • Benki ya TADB yatoa mkopo Sh7.7 bilioni kuwalipa wakulima. 

Dar es Salaam. Wakati msimu wa ununuzi wa kahawa kwa mwaka 2020/21 ukizinduliwa katika mkoa wa Kagera, wanunuzi wametakiwa kuzingatia bei elekezi ya Sh1,200 kwa kilo na kuhakikisha wanafanya biashara hiyo kwa uwazi ili kulinda maslahi ya wakulima. 

Bei hiyo elekezi itakayotumika mkoani humo ni kwa ajili ya kahawa ya maganda ambayo haijakobolewa. 

Hiyo ni tofauti na pamba ambapo Serikali imesema haitahusika kupanga bei bali nguvu ya soko itaamua.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti amewataka wanunuzi wa kahawa kufanya biashara hiyo mchana bila kuwahujumu wakulima kwa kuwa kahawa ni biashara halali na hakuna sababu ya kuuzwa gizani.

“Fanyeni biashara hii mchana kweupe maana hata wakulima wanavuna mchana kweupe, nielekeze tu katika mkoa wa Kagera sitaruhusu biashara ya kahawa kufanyika usiku hii siyo biashara haramu,” amesema Brigedia Jenerali Gaguti. 

Mpaka sasa, amesema wamepokea maombi ya wafanyabiashara nane na kuwataka wafanyabaiashara wengine ambao wako tayari kununua kahawa kwa bei nzuri kujitokeza na kutangaza bei ili wapatiwe kahawa.


Soma zaidi:


Mkuu huyo wa mkoa aliyekuwa akizungumza Jumanne katika Chama cha Msingi cha Mabira wilayani Kyerwa, amewataka wakulima kutunza ubora wa kahawa yao kabla ya kuipeleka katika  vyama vya msingi ili kuhakikisha kahawa kutoka Kagera inafika sokoni na ubora unaotakiwa.

Katika msimu huu 2020/21 mkoa huo unatarajia kukusanya takribani kilo milioni 60 ya kahawa juu ya kiasi cha msimu uliopita cha kilo milioni 52. 

Mtendaji Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) Japhet Justine amesema msimu huu wa 2020/21 tayari wameweka Sh7.7 bilioni  katika akaunti za vyama vikuu vya ushirika vya KDCU Limited na KCU 1990 Limited mkoani humo kwa ajili ya kukusanya kahawa ya wakulima na bila kuchelewesha malipo yao. 

Fedha hizo ni mkopo ambao utatozwa riba ya asilimia 9 kutoka asilimia 12 iliyokuwa inatozwa awali. 

Bodi ya Kahawa Tanzania tayari imetoa tangazo la kufunguliwa kwa msimu wa ununuzi wa kahawa ambalo linatoa mambo ya msingi ya kuzingatia ikiwemo ununuzi kufanyika katika minada ya kanda.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Rais Samia: Kalamu yangu ina hatari, sijawahi kusaini mtu kunyongwa

Nukta TV

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Rais Samia: Matumizi jina Samia, likiwa kila mahali inachosha, tafuteni wengine

Nukta TV