Wananchi wanavyoweza kuwasimamia viongozi wao wa kijiji
- Ni pamoja na kuwaondoa madarakani viongozi wa kijiji/mtaa ambao si waadilifu.
Dar es Salaam. Katika majukumu ya kijiji/mtaa wananchi wanapaswa kufahamu kuwa wana wajibu wa kuwasimamia viongozi wao katika ngazi hiyo ili kupata maendeleo yanayokusudiwa.
Usimamizi wa wananchi kwa viongozi hao ni pamoja na kuhakikisha wanachagua viongozi bora watakaowatumikia na kutimiza majukumu yao kiuadilifu.
Vilevile, wananchi wana wajibu wa kuhoji utendaji wa viongozi wao kupitia vikao mbalimbali vya kijiji/mtaa, na kuwaondoa madarakani viongozi wasiowajibika.
Ikiwa wananchi watawasimamia viongozi wa kutimiza majukumu yao, itasaidia kuharakisha maendeleo ya kijiji na matumizi sahihi ya rasilimali zao.

Latest