Faida za wananchi kushiriki katika maendeleo ya kijiji

February 3, 2022 6:19 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Huu ni mchakato unaohusu kuhusika na kuhusishwa kwa mwananchi katika Upangaji Utekelezaji, Usimamizi na Tathmini ya mipango mbalimbali ya maendeleo katika kijiji au mtaa. 

Vilevile kushiriki kutambua changamoto na kuweka  vipaumbele ili kuibua miradi mbalimbali ya maendeleo na kuweka mikakati ya utekelezaji katika ngazi ya kijiji/mtaa. Ushiriki na Ushirikishwaji wa wananchi ni fursa ambayo mwananchi anapaswa kuitambua na kuifaidi ili kuleta tija kwenye maisha yake na jamii yake.

Fursa anazopata mwananchi zinaweza kuwa za kiraia ,kiuchumi ,kijamii  na kiutendaji. Fursa ya kiraia ni kushiriki katika vikao rasmi vya maamuzi, kuchagua na kuchaguliwa kuwa kiongozi.

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW