Wanahabari wa Tanzania, Kenya kukutana jukwaa moja la tabianchi Ghana

February 14, 2019 10:02 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Wewe ni Mwanahabari unapenda kufaidika na fursa za mafunzo ya kuendeleza taaluma yako? Shirikia lisilokuwa la Kiserikali la Hivos litawakutanisha Wanahabari kutoka nchi za Kenya na Tanzania, katika kipindi cha wiki moja kuwajengea uwezo katika masuala ya tabianchi na mazingira. 

Muda huo utahusisha siku moja ya mafunzo; uwezekano wa kutembelea mradi mdogo wa kuzalisha umeme na siku tatu za kuhudhuria Mkutano wa Wiki ya Tabianchi Afrika (Africa Climate Week) utakaofanyika kati ya Machi 18-22, 2019 Jijini Accra, Ghana.na kuwahusisha wadau mbalimbali wa sekta ya umma na binafsi. 

Washiriki wa mkutano huo watajikita zaidi kuibua mbinu zitakazosaidia ushirikiano baina ya wadau katika sekta mahususi kama nishati, kilimo na maendeleo ya makazi.

Mwanahabari wa aina gani unayehitajika?

  • Umewahi kupata mafunzo na Hivos na umezalisha habari kuhusu nishati jadidifu baada ya mafunzo.
  • Unapenda sana kuripoti masuala ya nishati jadidifu ama mabadiliko ya tabianchi.
  • Utakuwa tayari kutengeneza mpango wa uzalishaji habari kabla ya mkutano na kuzalisha habari wakati na baada ya mkutano.

Kama ni miongoni mwa Wanahabari wenye sifa hizo basi hiyo ni fursa muhimu kwako. Kufahamu zaidi jinsi ya kutuma maombi na maelezo muhimu soma zaidi hapa.  

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
26 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
26 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
26 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV