Walioomba ajira Jeshi la Polisi Tanzania waitwa kwenye usaili

April 23, 2025 5:50 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Zoezi la usaili litaanza rasmi tarehe 28 Aprili hadi 11 Mei 2025.
  • Kila msailiwa anatakiwa kufika na vyeti halisi vya taaluma, cheti cha kuzaliwa, pamoja na kitambulisho Taifa au namba ya NIDA.

Dar es Salaam. Jeshi la Polisi Tanzania limetangaza kuanza kwa zoezi la usaili kwa vijana waliotuma maombi ya kujiunga na Jeshi hilo kupitia mfumo wake wa maombi ya ajira (Tanzania Police Force Recruitment Portal) . 

Usaili huo utafanyika kuanzia tarehe 28 Aprili hadi 11 Mei 2025 katika maeneo mbalimbali nchini.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali (IGP) Camillus Wambura, wasailiwa wenye elimu ya Shahada, Stashahada na Astashahada watafanyiwa usaili jijini Dar es Salaam katika uwanja wa gwaride uliopo kambi ya polisi, barabara ya Kilwa nyuma ya kituo cha Polisi Kilwa Road.

Wasailiwa watakaofika baada ya tarehe 28 Aprili 2025 hawatapokelewa. Picha | Ajira ya leo.

Kwa upande wa wasailiwa wenye elimu ya kidato cha nne na sita, usaili utafanyika katika mikoa waliyoweka kama chaguo wakati wa kutuma maombi, chini ya usimamizi wa Makamanda wa Polisi wa mikoa husika.

Aidha, kwa wasailiwa wa Zanzibar wa elimu zote kuanzia kidato cha nne hadi Shahada usaili utafanyika kwenye maeneo yaliyopangwa kulingana na mikoa. 

Kwa walio Unguja, usaili utafanyika Makao Makuu ya Polisi Zanzibar (Ziwani), wakati walio Pemba watafanyiwa usaili katika Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba, Chakechake.

Jeshi la Polisi limeelekeza kuwa kila msailiwa anatakiwa kufika na vyeti halisi vya taaluma, cheti cha kuzaliwa, kitambulisho cha Taifa cha NIDA au namba ya NIDA, pamoja na mavazi ya michezo. 

Hata hivyo taarifa hiyo imeonya kuwa wasailiwa watakaofika baada ya tarehe 28 Aprili 2025 hawatapokelewa.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
7 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
7 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV