Wagonjwa wa Corona wafikia 24 Tanzania

April 6, 2020 2:27 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Visa vingine vingine vinne vimethibitishwa leo na Wizara ya Afya.
  • Wagonjwa hao wako Dar es Salaam, Mwanza na Zanzibar. 
  • Serikali yawataka wananchi kuendelea kuchukua tahadhari ya kujikinga. 

Dar es Salaam. Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amesema kuna ongezeko la wagonjwa wengine wanne wa Corona kutoka Dar es Salaam, Mwanza na Zanzibar na kufanya idadi ya walioambukizwa ugonjwa huo kufikia 24 tangu ulipoingia nchini katikati ya Machi 2020. 

Mwalimu wameeleza katika taarifa yake leo (Aprili 6, 2020) kuwa wagonjwa hawo ni pamoja na wagonjwa wawili waliotolewa taarifa jana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Kati ya wagonjwa wapya wawili, Mwalimu amesema mmoja ni mwanaume (41), Mtanzania na mfanyabiashara mkazi wa Mwanza aliyeingia nchini akitokea Dubai Machi 24, 2020 kupitia uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) na Machi 29 alielekea Mwanza ambapo alichukuliwa vipimo na kukutwa na maambukizi ya Corona.

Mgonjwa huo anauingiza Mwanza katika orodha ya mikoa iliyorekodi wagonjwa wa virusi vya corona hadi sasa ukiwemo mkoa wa jirani wa Kagera.  

“Mgonjwa mwingine ni mwanaume mwenye umri wa miaka 35, raia wa Tanzania mkazi wa Dar es Salaam, mfanyabiashara.

“Wagonjwa wote wako chini ya uangalizi wa watoa huduma za afya katika vituo maalum vya tiba Dar es Salam, Mwanza na Zanzibar,” inasomeka sehemu ya taarifa hiyo.


Zinazohusiana


Aidha, Wizara ya Afya imesema inaendelea kuwafuatilia kwa karibu watu wote waliowahi kukutana na watu hao ili kudhibiti maambukizi mapya ya Corona. 

Mpaka sasa Tanzania imethibitisha kifo cha mtu mmoja aliyefariki kwa ugonjwa huo huku watatu akipona.

Hata hivyo, wananchi wametakiwa kuendelea kuchukua tahadhari ya kunawa mikono mara kwa mara, kutokugusa pua, mdomo au macho, kutumia tishu wakati wa kukohoa au kupiga chafya na kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
16 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
16 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
16 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Magonjwa haya matano yanayoongoza kwa kuua watu duniani

Nukta TV

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Mambo yakuzingatia kabla ujawasha gari lako asubuhi

Nukta TV

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Kutana na ‘Poultry Plucker’, mashine inayonyonyoa kuku watatu kwa dakika moja

Nukta TV