Wafanyabiashara wa mchele tabasamu tupu Njombe

May 11, 2020 2:28 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Bei ya jumla ya zao hilo ni zaidi ya mara mbili ya inayotumika Shinyanga, Tabora, Dar es Salaam na mji wa Mpanda ambayo ni Sh100,000. 
  • Wafanyabiashara wa Njombe wanauza maharage kwa Sh250,000 bei ya jumla.

Dar es Salaam. Wafanyabiashara wa mchele katika Mkoa wa Njombe leo watalala na tabasamu baada ya bei ya jumla inayotumika kuuza za hilo kuwa zaidi ya mara mbili ya ile ya mikoa ya Shinyanga, Tabora, Dar es Salaam na mji wa Mpanda. 

Mchele ni miongoni mwa mazao makuu ya chakula yanayotegemewa na Watanzania kwa ajili ya matumizi mbalimbali ikiwemo chakula. 

Takwimu za mazao makuu ya chakula zilizotolewa na Wizara ya Viwanda na Biashara leo (Mei 11, 2020) zinaonyesha kuwa gunia la kilo 100 la mchele linauzwa kwa Sh250,000 Njombe, jambo linalofaidisha zaidi wafanyabiashara na wakulima wanaouza zao hilo katika mkoa huo.  

Bei hiyo ya jumla ni mara mbili zaidi ya ile ya Sh100,000 inayotumika katika mikoa ya Shinyanga, Tabora, Dar es Salaam na mji wa Mpanda. 

Hata hivyo, bei inayotumika Njombe ndiyo bei ya juu kabisa ya zao hilo nchini ikilinganishwa na mikoa mingine huku inayotumika Shinyanga, Tabora, Dar es Salaam na mji wa Mpanda ndiyo bei ya chini kabisa. 

Bei ya juu ya leo imepanda kidogo ikilinganishwa na ya Ijumaa Mei 8 iliyorekodiwa katika Mkoa wa Lindi ambapo gunia la kilo 100 la maharage lilikuwa linauzwa kwa Sh 246,000. 

Kwa mujibu wa wizara hiyo, ijumaa kulikuwa hakuna takwimu za mazao za Mkoa wa Njombe. 

Bei ya chini imebaki kama ilivyokuwa Ijumaa isipokuwa imeongezeka mikoa miwili ya Dar es Salaam na Tabora na mji wa Mpanda ambayo inatumia bei hiyo.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.