Wafanyabiashara Kariakoo watii maagizo wahama barabarani

February 17, 2026 11:22 am · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Wafanyabiashara wa ndani ya soko wasema uwepo wa wafanyabiashara wanomwaga bidhaa nje ya soko unafanya wateja wengi kuishia nje jambo linalowakosesha mapato na wateja.

Dar es Salaam. Wafanyabiashara wa soko la kimataifa la Kariakoo wametii maagizo yaliyotolewa na viongozi mbalimbali wa serikali yaliyowataka kuacha kufanya biashara maeneo yasiyoidhinishwa ikiwemo barabarani.

Nukta Habari ilipita katika baadhi ya mitaa inayozunguka soko hilo ambayo awali ilikuwa imezongwa na wafanyabiashara hao na kujionea barabara zikiwa tupu bila misongongamano hiyo.

Hayo yanajiri ikiwa ni siku nane tangu soko hilo lizunduliwe na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan Februari 8, 2026 baada ya takribani miaka mitano tangu soko hilo liteketee kwa moto Julai 10, 2021. 

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wafanyabiashara wa ndani ya soko hilo wanasema kuwepo kwa wafanyabiashara wanomwaga bidhaa nje ya soko kunafanya wateja wengi kuishia nje jambo linalowakosesha mapato na wateja.

Katibu Msaidizi na kiongozi wa sakafu ya ardhini ‘Ground Floor” wa soko hilo Thomas Philipo ameiambia Nukta Habari kuwa kuwepo wa wafanyabiashara wanaopanga bidhaa nje ya soko kunachangia wanunuzi wa bidhaa kuishia nje na hivyo kulikosesha soko na wafanyabiashara ambao wanalipa kodi kwa Serikali mapato. 

Hata hivyo, licha kuonekana wafanyabiashara hao wametii maagizo ya viongozi Nukta Habari imeshuhudia Jeshi la Polisi likifanya doria wakati wote kuzunguka soko hilo ambapo kwa mujibu wa Philipo doria hiyo ni kwa ajili ya kukamata yeyote atakayepanga bidhaa katika maeneo yasiyoruhusiwa ukiachilia mbali ulinzi na usalama wa soko.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...

Enable Notifications OK No thanks