Wafahamu wanafunzi 10 bora mtihani darasa la saba mwaka 2020

November 21, 2020 10:39 am · Nuzulack Dausen
Share
Tweet
Copy Link
  • Msichana kutoka Graiyaki awatakisa wavulana baada ya kuongoza kitaifa.
  • Shule ya Kwema Modern iliyopo mkoani Shinyanga yaingiza wanne kwa mpigo. 

Dar es Salaam. Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) limemtangaza Herrieth Josephat kutoka Shule ya Msingi ya Graiyaki mkoani Mara kuwa ndiyo mwanafunzi bora kitaifa katika mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2020 uliofanyika mapema Oktoba mwaka huu.

Herrieth ndiyo mwanafunzi pekee wa kike katika orodha ya wanafunzi 10 bora kitaifa iliyotangazwa leo Novemba 21, 2020 jijini Dar es Salaam na Katibu Mtendaji wa baraza hilo Dk Charles Msonde.

Herrieth anafuatiwa kwa karibu na Huma Huma kutoka Kwema Modern iliyopo mkoani Shinyanga pamoja na Gregory Alphonce kutoka Twibhoki mkoani Mara. 

Wanafunzi wengine katika 10 hiyo bora ya mwaka 2020 ni Nyambina Nyambina wa Graiyaki, Andrew Mabula wa Kwema Modern, na Jonas Ayubu wa Little Flower iliyopo pia mkoani Mara.


Soma zaidi: 


Katika orodha hiyo ya dhahabu wapo pia Emmanuel Paul na Emmanuel Marwa wa Kwema Modern, Prosper Tumbo na Yesaya Bendera wote wa God’s Bridge iliyopo mkoani Mbeya.

Shule ya Kwema Modern ndiyo imetawala zaidi katika orodha ya wanafunzi 10 bora kitaifa baada ya kuwa na wanafunzi wa nne katika kinyang’anyiro hicho cha juu ikifuatiwa kwa karibu na Graiyaki ya Mara na God’s Bridge ambazo zimeingiza wanafunzi wawili wawili kila moja.

Wanafunzi nane kati ya 10 walioingia katika orodha ya 10 bora mwaka huu wanatoka katika shule za msingi zilizopo katika mikoa ya Kanda ya Ziwa ya Mara na Shinyanga. Mbeya ndiyo mkoa pekee uliowakilishwa katika orodha hiyo yenye wanafunzi wenye ufaulu wa juu zaidi nchini.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
8 Sep, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
8 Sep, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwanzo, mwisho sikia wasifu wa mume wa Rais Samia, Hafidh Ameir.

Mwanzo, mwisho sikia wasifu wa mume wa Rais Samia, Hafidh Ameir.

Nukta TV

Viongozi wa nchi, walivyomzika mume wa Rais Samia, Hafidh Ameir

Viongozi wa nchi, walivyomzika mume wa Rais Samia, Hafidh Ameir

Nukta TV

Mume wa Rais Samia, Hafidh Ameir Hassan afariki dunia leo Septemba 07, 2026

Mume wa Rais Samia, Hafidh Ameir Hassan afariki dunia leo Septemba 07, 2026

Nukta TV