NECTA yatangaza matokeo darasa la saba 2020

Mwandishi Wetu 0425Hrs   Novemba 21, 2020 Habari
  • Shule gani zimekuwa kinara mwaka huu?
  • Wanafunzi wa kike wamefanya vipi mwaka 2020?

Dar es Salaam. Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) limetangaza matokeo ya mtihani wa darasa la saba mwaka 2020 ikiwa ni miezi miwili baada ya watoto hao kuhitimu elimu ya msingi Septemba mwaka huu.

Matokeo hayo yametangazwa leo Novemba 21, 2020 na tayari yameshapakiwa katika tovuti ya baraza hilo www.necta.go.tz.

Mtihani wa darasa la saba ni hatua muhimu katika safari ya elimu ya sekondari na hatimaye elimu ya juu nchini.

Tutakuletea undani wa matokeo yote hayo hivi punde yaliyochambuliwa kwa kina zikiwemo shule 10 bora na wanafunzi waliotikisa mwaka huu.

Related Post