Dk Gladness Salema achaguliwa na CCM kugombea ubunge EALA 

September 2, 2024 7:50 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  • Atapigiwa kura Septemba 5, 2024 kuwania nafasi hiyo.
  • Ni safari ya kumtafuta mrithi wa Dk Shongo Sedoyeka aliyefariki dunia Juni 13, 2024.

Dar es Salaam. Kamati ya wabunge wa Chama cha Mapinduzi ( CCM) imemchagua Dk Gladness Salema kukiwakilisha chama hicho katika uchaguzi wa mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) utakaofanyika Septemba 5, 2024 bungeni.

Dk Gladness ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), amewashinda wapinzani wake wawili kwa kura 139 dhidi ya 53 za Lucia Pande na 52 za Queenelizabeth Makune.

Uchaguzi huo uliofanyika leo Jumatatu Septemba 2, 2024 katika ukumbi wa NEC White House, unalenga kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Dk Shongo Sedoyeka aliyefariki dunia Juni 13, 2024.

Wajumbe wa CCM wakiwa katika mchakato wa kumchagua mbunge wa kuwawakilisha chama hicho katika uchaguzi wa mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki.Picha l CCM

Kabla ya kuanza kwa uchaguzi huo, msimamizi wa uchaguzi huo, Issa Haji Gavi alitangaza wabunge watapigia kura majina tisa kwa awamu ya kwanza, ili kupata washindi watatu.

Majina hayo tisa yaliyopigiwa kura ni kati ya wana CCM 10 walioteuliwa na chama hicho kugombea nafasi hiyo ambapo mmoja alijitoa kwenye kinyang’anyiro hicho.

Wengine waliokuwa wakigombea nafasi hiyo ni Maria Sebastian, Ester Chaula aliyejitoa, Prof Neema Kumburu, Fatma Kange, Hawa Mkwela, Fatuma Msofe na Theresia Dominic.

Wabunge wa EALA huchaguliwa kwa kipindi cha miaka mitano na wanaweza kuchaguliwa tena kwa kuteua wawakilishi wa nchi wanachama katika Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ambazo ni Kenya, Tanzania, Uganda, Rwanda, Burundi, Sudan Kusini, Somalia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
13 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV