Vodacom yawekeza Sh11 bilioni huduma za jamii Tanzania

June 27, 2019 3:35 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Uwekezaji huo umefanyika kupitia taasisi yake ya Vodacom Tanzania Foundation kati ya mwaka 2014 na 2017. 
  • Wanakusudia kuwekeza tena Sh1 bilioni kila mwaka kwenye elimu na mazingira.
  • Wamejikita zaidi kuinua maisha ya watoto na wanawake kupitia sekta za afya, elimu na kilimo.
  • Serikali yasema itaendelea kushirikiana nao kwa kuwawekea mazingira mazuri ya biashara. 

Dar es Salaam. Kampuni ya simu ya Vodacom Tanzania imesema katika kipindi cha miaka mitano iliyopita iliwekeza Sh11 bilioni katika sekta mbalimbali ikiwemo afya zilizogusa na kuboresha maisha ya wananchi wenye uhitaji katika jamii. 

Kampuni hiyo inayosimamia taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation imesema katika kipindi cha mwaka 2019 na 2021 inakusudia kuwekeza Sh1 bilioni kila mwaka kwa ajili ya kuwasaidia wananchi hasa wanawake na watoto wa hali ya chini. 

Mkurugenzi wa  taasisi hiyo, Rosalynn Mworia  amesema kiasi hicho cha Sh11 bilioni kilitolewa kati ya mwaka 2014 na 2017 ikiwa ni jitihada za mfuko huo kuisaidia jamii yenye uhitaji. 

Akizungumza katika uzinduzi wa ripoti ya matokeo ya Vodacom kwa jamii (Social Impact Report and new strategy to deliver inclusive growth) leo Juni 27, 2019, Jijini Dar es Salaam, amesema kupitia sekta za elimu, afya na kilimo wamefanikiwa kuboresha maisha ya watu zaidi ya milioni tatu. 

“Hadi kufikia hapa tumeshawekeza Sh11 bilioni ambazo zimetuwezesha kuwafikia watoto wa kike na wanawake katika kuwasaidia kwenye afya pamoja na uchumi,” amesema Mworia.

Aidha, Mworia amesema mwaka 2019 hadi 2021  watawekeza zaidi katika elimu, uchumi na shughuli ambazo zitasaidia kutunza mazingira ambapo kila mwaka watatoa Sh1 bilioni. 

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-Tamisemi, Joseph Kandege, akikata utepe kuzindua Ripoti ya Jamii  kutoka Vodacom leo Jijini Dar es Salaam, kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Mawasiliana Tanzania (TCRA), Dk Jones Kilimbe, kutoka kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk Leonard Akwilapo, Mkurugenzi wa Taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation, Rosalynn Mworia na Mkurugenzi Mkuu wa Vodacom, Hashim Hendi. Picha|Maelezo.

Takwimu za mwaka 2018 za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) zinaonyesha Vodacom inaongoza kwa kuwa na wateja milioni 14.14 kati ya kampuni za simu saba zinazotoa huduma hiyo hapa nchini. 

Pia inaongoza pia kwa idadi ya wateja wa huduma za kifedha kupitia simu za mkononi kwa kuwa na asilimia 38.6 ya soko ikifuatiwa na kampuni za Tigo (Tigo Pesa) na Airtel (Airtel Money).


Soma zaidi:


 Akizungumza  katika hafla ya uzinduzi wa ripoti hiyo, Naibu  Waziri Ofisi ya Rais-Tamisemi, Joseph Kandege amesema Serikali itaendelea kushirikiana na kampuni za simu ikiwemo Vodacom ili kuwasaidia wananchi katika mambo mbalimbali ya kijamii ikiwemo ya afya, elimu  na miundombinu.

“Serikali itaimarisha miundombinu ili kuhakikisha Vodacom inawafikia  watu wenye uhitaji na pia tumeona jinsi walivyoweza kuwasaidia watoto wa kike na wakina mama wenye fistula kupata matibabu  ya ugonjwa huo na kugawa taulo kwa watoto wa kike wenye uhitaji, ambao wanakosa kwenda shuleni pindi wawapo kwenye hedhi,” amesema Kandege.

Amesema matarajio yake ni kuwa  kazi inayofanywa na vodacom  inaweza kufanywa na mashirika mengine kwa kushirikiana na kampuni hiyo ili kuifikia jamii kwa upana zaidi. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV