Vijana wazidi kutawala soko la mitandao ya kijamii Tanzania

February 9, 2019 2:16 pm · Zahara
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Kwa mujibu wa ripoti ya Dijitali ya Januari 2019 iliyotolewa kampuni ya We are social ya nchini Marekani inaeleza kuwa licha ya changamoto za usiri, udukuzi, habari za uongo na mambo mengine hasi ya maisha ya mtandaoni, bado dunia inaendelea kushikamana na intaneti na mitandao ya kijamii. 

Ukuaji wa matumizi ya mitandao duniani hauonyeshi dalili yoyote ya kupungua huku maelfu ya watu wakiingia mtandaoni kila siku. Ukuaji huo ndiyo unaochochea matumizi ya mitandao ya kijamii.

Ripoti hiyo iliyojikita kuangalia mwenendo wa matumizi ya mitandao ya kijamii hasa Januari mwaka huu, inaeleza kuwa watu bilioni 3.5 duniani ambapo ni sawa na kusema asilimia 45 ya idadi ya watu wote duniani wanatumia mitandao ya kijamii. Na kundi la vijana ndiyo vinara wa mitandao ya kijamii. 

Takwimu hizo zinaashiria kuwa dunia inazidi kujikita zaidi katika teknolojia, jambo linalotoa ujumbe hasa kwa vijana wa Tanzania kutafuta namna ya kufaidika na fursa hizo ili kuondokana na changamoto za ajira na umaskini wa kipato.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
26 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
26 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
26 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV