Utoaji chanjo ya Uviko-19 washika kasi Tanzania

November 2, 2021 11:37 am · Herimina
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Dorothy Gwajima ametangaza kuwa hadi kufikia Oktoba 31 Watanzania 88,546 walikuwa wamepata chanjo ya Sinopharm.

“Chanjo ya Johnson Jonhson iliisha tangu Oktoba 19, sasa tunatoa chanjo ya Sinopharm ambayo hadi jana watu 88,546 wameshapata chanjo hiyo sawa na asilimia 8.3 ya chanjo zilizoletwa,” amesema Novemba 2, 2021 katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNIA) wakati wa kupokea dozi 500,000 za chanjo ya Sinopaharm.

Dk Gwajima amesema kumekuwa na mwamko mzuri wa wananchi kuchanja huku ambapo ameitaja  mikoa 10 iliyofanya vizuri kwenye utoaji wa chanjo hiyo ya Ruvuma, Mbeya, Mtwara, Kagera, Dodoma, Arusha, Dar, Mwanza, Mara, Songwe na Pwani.

“Tutaanza kutoa takwimu za mikoa katika utoaji chanjo ili kutoa changamoto kwa mikoa ambayo iko chini,” amesema Dk Gwajima. 

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Kwanini uchafuzi wa mazingira ni tishio kwa afya ya binadamu na uchumi

Kwanini uchafuzi wa mazingira ni tishio kwa afya ya binadamu na uchumi

Nukta TV

Tunachokifahamu kuhusu ziara ya Rais Samia Urusi, kidiplomasia na uchumi

Tunachokifahamu kuhusu ziara ya Rais Samia Urusi, kidiplomasia na uchumi

Nukta TV

Kutoka Ubunge hadi mshauri wa Rais, Panda shuka ya Ummy Mwalimu katika siasa

Kutoka Ubunge hadi mshauri wa Rais, Panda shuka ya Ummy Mwalimu katika siasa

Nukta TV