Ukatili, kuchepuka: Sababu kuu wanandoa kupeana talaka

March 8, 2023 12:44 pm · admin
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Wakati  takwimu za Ripoti ya Utafiti wa Ufuatiliaji wa Kaya (NPS) 2020/2021 iliyotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), zikionyesha kuwa asilimia 57 ya Watanzania hawapo kwenye ndoa, sababu za wanaume na wanawake kutalikiana zimekuwa zikitofautiana. 

Ripoti ya Utafiti wa Taasisi za Kijamii na Jinsia (SIGI) ya mwaka 2021  imebainisha sababu ambazo zinaweza kusababisha wanandoa kutalikiana ama kutengana. 

Licha ya kuwa kila kundi la yaani wanawake na wanaume wameainisha sababu za kutalikiana, matendo kama kuzini nje ya ndoa, pamoja na ukatili yameonekana kuwa na asilimia nyingi za kuwa sababu ya talaka au wanandoa kutengana.


Enable Notifications OK No thanks