Ufahamu mlima uliotengenezwa kwa taka za kielektroniki

December 18, 2021 4:39 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Mlima huo watengenezwa ili kuwakumbusha watu uharibifu unaosababishwa na teknolojia.
  • Mbali na taka, mlima huo una sura za viongozi wa mataifa saba yaliyoendelea zaidi katika viwanda.
  • Hadi sasa taka zaidi ya tani 50 zimezalishwa duniani.

Joe Rush, mbunifu kutoka Uingereza, ametengeneza mlima kwa kutumia taka za kielektroniki akiwa na lengo la kukumbusha watu na nchi zilizoendelea kwa sekta ya viwanda kurejelea taka ambazo zinatokana na bidhaa wanazozizalisha ikiwemo simu, kompyuta na deki.

Mlima huo wa taka uliopo nchini Uingereza umetengenezwa kwa kutumia malighafi ya plastiki, nyaya na mabaki ya bidhaa za kielektroniki ambazo zimeharibika na hazina kazi tena.

Mlima huo uitwao “Recyclemore” ambao kwa tafsiri ya Kiswahili ni “rejelea zaidi” umetengenezwa ukiwa na mfanano wa sura saba za viongozi wanaotokea katika nchi zilizoendelea kiviwanda duniani ikiwemo Ufaransa, Japan, Italia, Canada, Marekani na Ujerumani.

Viongozi hao ni pamoja na Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson, Waziri Mkuu wa Japan Yoshihide Suga, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, Waziri Mkuu wa Italia Mario Draghi, Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau, Kansela wa Ujerumani Angela Merkel na Rais wa Marekani, Joe Biden.

Mlima huo umetengenezwa kwa mfanano wa sura za viongoozi wa mataifa saba ambayo yameendelea kiuchumi (G7) akiwemo Rais wa Marekani Joe biden. Picha| Mtandao.

Rush amesema mlima huo utawakumbusha viongozi hao na dunia kwa ujumla uharibifu ambao umefanywa na unaendelea kufanywa na taka za kielektroniki.

Mlima “Recyclemore” umetengenezwa kuhamasisha nchi zilizoendelea kiviwanda kutengenza bidhaa zinazokaa kwa muda mrefu, zinazoweza kurejelewa na kupunguza uzalishaji wa matoleo mapya.

Mlima huo umechukua nguvu ya watu 12 kuujenga ndani ya wiki sita.

Ripoti ya hivi karibuni ya Umoja wa Mataifa (UN) imesema zaidi ya tani milioni 53 za taka za kielektroniki zimetelekezwa duniani hadi kufikia mwaka 2019 ikiwa ni ongezeko la zaidi ya tani milioni tisa zilizozalishwa mwaka 2014.

“Recyclemore” utawakumbusha viongozi na dunia kwa ujumla uharibifu wa kimazingira unaosababishwa na bidhaa za kielektroniki. Picha| Mtandao.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Sep, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Sep, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴 LIVE: WABUNGE WAKIMCHAPA MASWALI MAZITO WAZIRI MKUU BUNGENI

🔴 LIVE: WABUNGE WAKIMCHAPA MASWALI MAZITO WAZIRI MKUU BUNGENI

Nukta TV

CEO, TAB Group: Africa Agri Expo 2026 inakwenda kufungua fursa kimataifa, kilimo cha Tanzania

CEO, TAB Group: Africa Agri Expo 2026 inakwenda kufungua fursa kimataifa, kilimo cha Tanzania

Nukta TV

TANTRADE: Tumieni vifungashio vya "Made in Tanzania"

TANTRADE: Tumieni vifungashio vya "Made in Tanzania"

Nukta TV