TCU yafungua dirisha udahili vyuo vikuu 2026/27, yaonya matapeli 

July 11, 2026 2:46 pm · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Dirisha hilo la awamu ya kwanza litadumu kwa muda wa mwezi mmoja kuanzia Julai 10 hadi Agosti 10, 2026.

Dar es Salaam. Vijana wenye mpango wa kujiunga na elimu ya juu nchini watakuwa na mwezi mmoja wa kupambania ndoto zao baada ya tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) kufungua dirisha la maombi ya udahili kwa mwaka wa masomo 2026/2027.

Dirisha hilo la awamu ya kwanza linalotarajiwa kuanza Julai 10 hadi Agosti 10, 2026 ambapo watu wote wanaotaka kujiendeleza kielimu watatakiwa kuwasilisha maombi ya udahili kwenye vyuo wanavyovipenda. 

Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Charles Kihampa, aliyekuwa akizungumza na wanahabari, amesema dirisha hilo linawahusu waombaji wenye sifa za kujiunga kupitia makundi matatu wakiwemo waliomaliza kidato cha sita. 

Sehemu kubwa ya kundi hili ni lile ambalo lilipata matokeo wiki hii ambao kwa mujibu wa Baraza la Mitihani (Necta) ufaulu wao kwa mwaka 2026 uliongezeka hadi kufikia asilimia 99.94.

“Kundi la pili ni wenye sifa stahiki za Stashahada kwa maana ya diploma au sifa nyingine linganifu, na kundi la tatu ni wenye sifa stahiki za cheti cha awali kinachotolewa na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania,” amesema Prof Kihampa.

Mambo ya kuzingatia kabla ya kuomba

Kabla ya kuwasilisha maombi, TCU imewataka waombaji kuzingatia mambo mbalimbali ikiwemo kusoma kitabu cha mwongozo wa udahili ili kujiridhisha kuwa wanakidhi vigezo vya programu wanazokusudia kuomba kabla ya kuwasilisha maombi yao. 

Aidha, mwombaji anatakiwa kutuma maombi moja kwa moja katika vyuo vikuu anavyohitaji kupitia mifumo ya kielektroniki ya kila chuo kulingana na taratibu zilizowekwa na taasisi husika.

Kabla ya kufanya hivyo mwombaji anashahuriwa kuhakikisha ametembelea tovuti za vyuo hivyo ili kupata taarifa za kina kuhusu programu za masomo, masharti ya udahili na utaratibu wa kutuma maombi kabla ya kufanya uchaguzi wa masomo.

Kwa waombaji wenye uraia wa Tanzania walio na vyeti kutoka nje wanatakiwa kupata ithibati ya ulinganifu wa vyeti hivyo kutoka TCU  kabla ya kuomba udahili.

Aidha, vyeti vya elimu ya sekondari vinapaswa kuthibitishwa na Necta pamoja na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET).

Epuka madalali

Ilikuepuka udanganyifu na kutapeliwa TCU imewataadharisha waombaji kujiepusha na watu wanaojitambulisha kama mawakala au washauri wanaoweza kusaidia kupata nafasi za udahili.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
11 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
11 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
11 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hawa ndio wanasoka 5 wanaoingiza mkwanja mrefu zaidi duniani

Hawa ndio wanasoka 5 wanaoingiza mkwanja mrefu zaidi duniani

Nukta TV

130 wakamatwa kwa tuhuma za kupanga na kuhamasisha uhalifu Tanzania

130 wakamatwa kwa tuhuma za kupanga na kuhamasisha uhalifu Tanzania

Nukta TV

Mfumuko wa bei Tanzania wapungua kwa 0.2%

Mfumuko wa bei Tanzania wapungua kwa 0.2%

Nukta TV