Tatizo la afya ya akili sasa kutupiwa macho
Dar es Salaam. Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema ipo haja ya kuwa na vituo maalumu vya kutoa huduma ya saikolojia pamoja na huduma za matibabu ya matatizo ya afya ya akili nchini Tanzania kutokana na mfululizo wa matukio yanayohusishwa na suala hilo.
Waziri Ummy aliyekuwa akizungumza katika kongamano la kwanza la kitaifa la afya ya akili lililofanyika Octoba 10,2022 ikiwa ni siku ya afya ya akili duniani alisema vituo hivyo vya saikolojia vitasaidia kupunguza wimbi watu kupata magonjwa ya akili.
Waziri wa Afya Mhe. @ummymwalimu amewataka Wataaalam wa Afya Nchini kujadili kuhusu kujumuisha Huduma za Saikolojia ya Afya ya Akili katika kwa huduma zitolewazo na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya @nhiftz
pic.twitter.com/882wX09RrG— Wizara ya Afya Tanzania ?? (@wizara_afyatz) October 10, 2022
Takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) zinabainisha kuwa mtu mmoja kati ya watu nane duniani anakabiliwa na tatizo la afya ya akili huku Tanzania ikiwa na takribani watu milioni saba wenye matatizo mbalimbali ya afya ya akili.

Latest