Tatizo la afya ya akili sasa kutupiwa macho

October 11, 2022 8:23 am · admin
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema ipo haja ya kuwa na vituo maalumu vya kutoa huduma ya saikolojia pamoja na huduma za matibabu ya matatizo ya afya ya akili nchini Tanzania kutokana na mfululizo wa matukio yanayohusishwa na suala hilo.

Waziri Ummy aliyekuwa akizungumza katika kongamano la kwanza la kitaifa la afya ya akili lililofanyika Octoba 10,2022 ikiwa ni siku ya afya ya akili duniani alisema vituo hivyo vya saikolojia vitasaidia kupunguza wimbi watu kupata magonjwa ya akili.

Takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) zinabainisha kuwa mtu mmoja kati ya watu nane duniani anakabiliwa na tatizo la afya ya akili huku Tanzania ikiwa na takribani watu milioni saba wenye matatizo mbalimbali ya afya ya akili.

 

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW