Tanzania kuunganisha mifumo ya uwekezaji kielektroniki

May 27, 2021 10:56 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Imeanza kufanya maboresho ya huduma za uwekezaji  kwa kuunganisha mifumo ya kielektroniki kwa taasisi na idara 11 za Serikali.
  • Itasaidia kurahisisha utoaji wa vibali na leseni za uwekezaji nchini.

Dar es Salaam. Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimeanza kufanya maboresho ya huduma za uwekezaji  kwa kuunganisha mifumo ya kielektroniki kwa taasisi na idara 11 za Serikali zinazotoa huduma kwenye kituo cha pamoja cha uwekezaji.

Maboresho hayo yatasaidia kurahisisha utoaji wa vibali na leseni za uwekezaji kwa kuunganisha mifumo hiyo ili kuwa na dirisha moja la uwekezaji nchini.

Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Dk Maduhu Kazi amesema maboresho hayo yatasaidia kuongeza ufanisi katika kutoa huduma kwa wawekezaji na kuimarisha utendaji kazi wa kituo hicho.

“Kama mnavyofahamu, Mheshimiwa Rais (Samia Suluhu Hassan) alitoa maelekezo ya namna ya kuboresha huduma za uwekezaji, kikao hiki ni muendelezo wa utekelezaji wa majukumu hayo, tulishaanza kuyafanyia kazi, na sasa tunaendelea, lengo ni kutoa huduma bora zaidi za uwekezaji” amesema Dk Kazi.

Dkt Maduhu amefanya kikao cha pamoja na  wakuu wa taasisi na idara za Serikali 11 zinazotoa huduma kwenye kituo cha huduma kwa wawekezaji cha pamoja (One Stop Facilitaion Centre) na kubainisha kuwa mchakato wa maboresho hayo unaendelea kufanyiwa kazi.


Zinazohusiana: 


Dk Kazi amepokea taarifa ya hatua ambazo zimechukuliwa kwa kila taasisi na idara husika zikiwepo kila taasisi kufungua mfumo wa kielektroniki kwa ajili ya utoaji vibali na leseni mbalimbali.

Maboresho haya yanaelezwa kuwa yatawawezesha wawekezaji wanaowekeza nchini kupata huduma kwa muda mfupi na kwa kutumia gharama ndogo.

Baadhi ya Taasisi zilizoshiriki katika kikao hicho ni pamoja na Uhamiaji, Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TMDA), Mamlaka ya Mapato Tanzani (TRA), Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira  (NEMC), Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi).

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV