Tanzania kuboresha huduma za afya kuhudumia watoto njiti

November 17, 2025 1:21 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  • Yasema inaimarisha miundombinu ya wodi maalumu na kutoa mafunzo kwa wahudumu wa afya.
  • Yatoa wito kwa wajawazito kuhudhuria kliniki na kujifungulia hospitali.

Dar es Salaam. Serikali ya Tanzania imesema inaendelea kuimarisha huduma za kuwatunza watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (njiti) ili kuboresha matunzo ya kitabibu, lishe na malezi kwa watoto hao wanapokuwa hospitalini na majumbani.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Novemba 17, 2025 na Wizara ya Afya imeeleza kuwa huduma zinazoimarishwa ni pamoja na miundombinu ya wodi maalum za watoto wachanga, kununua na kusambaza vifaa tiba, pamoja na kutoa mafunzo kwa wahudumu wa afya. 

Hayo yamebainishwa wakati ulimwengu unaadhimisha siku ya watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (World Prematurity Day) ikiwa lengo ni kuongeza uelewa wa jamii kuhusu changamoto zinazowakabili watoto njiti  ambao huzaliwa kabla ujauzito haujakamilisha wiki 37 za umri wa mimba.

Maadhimisho ya mwaka huu yanaongozwa na kaulimbiu isemayo, tuwapatie mwanzo bora watoto wachanga wanaozaliwa kabla ya wakati kwa afya bora ikiwa inalenga kuhakikisha kila mtoto njiti anapewa fursa ya kuishi, kukua na kustawi kwa kupata huduma stahiki za kitabibu, lishe bora, na uangalizi wa karibu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Shirika la Afya Duniani (WHO) takribani watoto milioni 15 huzaliwa kabla ya wiki 37 za ujauzito kila mwaka duniani, na zaidi ya watoto milioni moja hupoteza maisha kutokana na matatizo yanayohusiana na kuzaliwa kabla ya wakati.

WHO inasisitiza kuwa watoto njiti wako katika hatari kubwa ya kupata matatizo ya kiafya yanayohatarisha maisha kama shida ya kupumua, maambukizi na kushuka kwa joto la mwili.

Nchini Tanzania takwimu zinaonesha kuwa takribani mtoto mmoja kati ya 10 sawa na zaidi ya watoto 250,000 huzaliwa kabla ya wakati kwa mwaka, hali inayohitaji juhudi za pamoja katika kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto.

Hata hivyo, Wizara ya Afya imetoa wito kwa jamii kuhakikisha wajawazito wanahudhuria kliniki mapema na mara kwa mara, na kuhakikisha kila mama anajifungulia katika kituo cha kutolea huduma za afya ili kupunguza sababu za watoto kuzaliwa kabla ya wakati

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa wananchi kupima afya, kuacha uoga

Rais Samia Suluhu Hassan ametoa wito kwa wananchi kupima afya, kuacha uoga

Nukta TV

Uwepo wa vifaa, madaktari uendane na huduma inayotakiwa

Uwepo wa vifaa, madaktari uendane na huduma inayotakiwa

Nukta TV

Rais Samia: Maradhi ya moyo, saratani kwa watoto yaongezeka Tanzania

Rais Samia: Maradhi ya moyo, saratani kwa watoto yaongezeka Tanzania

Nukta TV