Tanzania inavyodhibiti migogoro ya binadamu na wanyamapori

April 6, 2022 5:17 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Inafanya doria za mara kwa mara katika maeneo yenye migogoro.

Dar es Salaam. Wizara ya Maliasili na Utalii imesema itaendelea kudhibiti migongano baina ya binadamu na wanyamapori katika maeneo ya kinga ya hifadhi na mtawanyiko wa wanyamapori mkoani Simiyu ili kupunguza athari ikiwemo uhalibifu wa mali na vifo vya watu.

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja amesema wizara yake hufanya doria za mara kwa mara kudhibiti wanyamapori wakali na waharibifu na pia vituo viwili vya askari vitajengwa katika maeneo ya Busega na Meatu mkoani humo.

Masanja ameyasema hayo Aprili 5, 2022 Bungeni jijini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Minza Mjika aliyetaka kufahamu mikakati ya Serikali kupunguza migogoro ya wanyamapori na binadamu.

Pia, wizara inatarajia kuajiri askari 600 na mafunzo ya mbinu za kujilinda na kukabiliana na wanyamapori wakali na waharibifu yametolewa kwa Halmashauri za wilaya 17 nchini.

Aidha, Wizara imetoa namba maalum za simu kwenye kila kanda za kiutendaji ili kuwezesha wananchi kutoa taarifa za matukio ya wanyamapori bila malipo.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
26 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
26 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
26 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV