Si kweli: TEC imetoa waraka kuhusu Uchaguzi Mkuu 2025

October 14, 2025 11:58 am · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • TEC imesema haihusiki na maudhui yeyote yaliyopo kwenye waraka huo feki na inasisitiza waumini na watanzania kuupuuza.

Dar es Salaam. Huenda ukawa ni moja ya watu waliokutana na chapisho katika mitandao ya kijamii linalodaiwa kuwa ni waraka uliotolewa na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) likitoa msimamo wa baraza hilo kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29.

Chapisho hilo feki limesambaa likiwa na nembo na mhuri wa baraza hilo pamoja na sahihi ya Rais wa TEC, Wolfgang Pisa pamoja na Katibu Mkuu, Padri Dk Charles Kitima likiwa na kichwa kinachosomeka ‘TAMKO LA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA (TEC) KUHUSU AMANI KWA TAIFA KUELEKEA SIKU YA UCHAGUZI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA UTAKAOFANYIKA TAREHE 29 OKTOBA 2025’.

Chapisho hilo ambalo pia liliripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari bila kuhakikiwa, limepokelewa kwa sura na mitazamo tofauti na baadhi ya wadau na kuzua mijadala katika mitandao ya kijamii kutokana na ajenda yake inayogusa moja kwa moja Uchaguzi Mkuu 2025.

Ukweli ni huu

TEC imekanusha  waraka huo na kusema ni batili na haujatolewa na baraza bali umetengenezwa na wapotoshaji kwa lengo la kupotosha.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Padri Dk Kitima imeeleza kuwa TEC haihusiki na maudhui yeyote yaliyopo kwenye waraka huo feki na kusisitiza waumini na watanzania kuupuuza.

“Tunapenda kuwatangazia waumini na watanzania wote kwa ujumla, kuwa waraka huo haukutolewa na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania,” imeeleza taarifa ya TEC

Aidha, TEC imeonya vikali na kuwataka wapotoshaji na wote wenye tabia ya kughushi taarifa kama hizo kukoma mara moja.

“Tabia hii mbaya ya kutumia Taasisi ya Maaskofu kupitisha jumbe zisizotokana na baraza ikomeshwe” imesisitiza TEC.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
WAMESANUKA, mbinu mpya ya usafirishaji wa dawa za kulevya yafichuliwa

WAMESANUKA, mbinu mpya ya usafirishaji wa dawa za kulevya yafichuliwa

Nukta TV

CCM yatoa ratiba maombi ya kumrithi Lukuvi, Israel, Lebanon wakisitisha mapigano

CCM yatoa ratiba maombi ya kumrithi Lukuvi, Israel, Lebanon wakisitisha mapigano

Nukta TV

Ridhiwani: Serikali inalenga kuacha tabasamu kwa watumishi wa Umma

Ridhiwani: Serikali inalenga kuacha tabasamu kwa watumishi wa Umma

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.