Si kweli: Mohammed Dewji amezindua sarafu mpya ya kidijitali Tanzania

February 6, 2025 11:44 am · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Asema akaunti yake ya X imedukuliwa akiwataka Watanzania kupuuzia ujumbe huo.

Dar es Salaam. Huenda umekutana na taarifa inayobainisha kuwa Bilionea na mfanyabiashara, Mohammed Dewji amezindua sarafu mpya ya kidijitali iitwayo  Tanzania Coin ($Tanzania), habari hiyo si ya kweli na unapaswa kuipuuza.

Taarifa hiyo ilichapishwa na kusambaa kupitia akaunti yake ya mtandao wa  X zamani Twitter jana Februari 5, 2025  ambapo sehemu ya chapisho hilo lilisomeka  “Nataka kuifanya Tanzania kuwa rejea ya kupitishwa kwa cryptocurrency, kama vile @nayibbukele alivyofanya kwa El Salvador.” 

Ujumbe huo ulifuatwa na chapisho jingine likisema, “Ni heshima kuwaletea watu ubunifu huu. Mustakabali wa fedha za kidijitali unaanza hapa.”

Akaunti ya Mo ya X imedukuliwa Watanzania watanzania wanatakiwa kupuuzia ujumbe huo, Picha | Kelvin Makwinya

Chapisho hilo lilifuatana na kiungo cha tovuti kinachodai kuelekeza watu kwenye maelezo ya jinsi ya kuwekeza kwenye sarafu hiyo na baadae ilichapishwa video ya mtu anayefanana na Mohamed Dewji akithibitisha kuwa akaunti yake haijaibiwa na yaya ndiye aliyeanzisha sarafu hiyo.

Watu wengi walipokea taarifa hizo kwa shauku, huku wengine wakihoji uhalali wake kupitia sehemu ya maoni na baadhi ya vyombo vya habari viliripoti tukio hilo kwa uzito wake kabla ya baadae kubainika ni jaribio la ulaghai.

Ukweli ni huu

Wakati Nukta Fakti ikiendelea kutafuta ufumbuzi wa taarifa hiyo saa mbili baadae kupitia akauti yake ya Instagram Mohammed Dewji alikanusha vikali taarifa hizo na kufichua kuwa akaunti yake ya X imedukuliwa. 

Katika ujumbe wake aliandika, “Akaunti yangu ya X imevamiwa. Tafadhali puuzia posti zozote au meseji zisizo za kawaida. Tunalifanyia kazi kwa haraka ili kurejesha usalama wa akaunti. Kaeni makini.”

Mpaka kufikia Februari 6, 2025, saa 3:00 asubuhi, akaunti yake ya X bado ilikuwa chini ya wadukuzi, wakiendelea kuchapisha ujumbe wa uongo na kutuma viungo vya tovuti na makundi ya Telegram yanayodai kutoa maelekezo ya uwekezaji kwenye Tanzania Coin.

Nukta Fakti inathibitisha kuwa taarifa za Mohammed Dewji kuzindua Tanzania Coin si za kweli. Ni jaribio la ulaghai mtandaoni linalolenga kuwadanganya watu wawekeze pesa zao kwenye mpango usio rasmi.

Pamoja na kwamba viongozi wa Serikali wamekuwa wakitoa matamko ya kuanzisha mifumo ya kusimamia sarafu za kidijitali bado haijatangazwa rasmi lini Tanzania itatambua na kuruhusu matumizi ya sarafu za kidijitali.

Viashiria vingine vya udanganyifu vilivyopo kwenye taarifa hiyo ni hakuna tangazo lolote rasmi kutoka kwa Mohammed Dewji kupitia vyanzo vyake halali kama tovuti yake, kampuni zake au vyombo vya habari kuhusu uwepo wa sarafu hiyo.

Aidha  machapisho hayo yana makosa ya kisarufi na uandishi jambo ambalo si la kawaida kwa ujumbe rasmi wa bilionea huyo.

Hata hivyo, kiungo cha tovuti kilichowekwa kwenye machapisho hayo hakina kikoa  cha usalama cha Serikali (gov) au cha kampuni rasmi, dalili ya kuwa ni jaribio la ulaghai mtandaoni.

Uchambuzi uliofanywa na Nukta Fakti umebaini pia kuwa video inayomuonesha mtu anayefanana na Dewji kuwathibitishia watu kuhusu urasmi wa sarafu hiyo ni ya kutengenezwa kwa kutumia akili unde (AI) na si halisi.

Wananchi wanashauriwa kuwa waangalifu na kuhakikisha wanapata taarifa kutoka vyanzo vya kuaminika kabla ya kuwekeza katika miradi yoyote ya fedha za kidijitali.

 Pia, ni muhimu kuripoti akaunti yoyote inayotilia shaka kwa mamlaka husika ili kusaidia kudhibiti uhalifu wa mtandaoni.

Kwasasa Mo Dewji amefanikisha kuirejesha akaunti yake ya mtandao wa X kwenye udhubiti wake na maeomba radhi kwa kufanya chapisho linalosomeka “Tunaomba radhi kwa usumbufu uliosababishwa na uvamizi wa akaunti yangu. Tumesha dhibiti hali, lakini tunawasihi kuwa makini na ulaghai na kuhakikisha mnapata taarifa sahihi kutoka vyanzo vyetu rasmi,” ameandika Mo Dewji.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
7 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
7 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

MFUMUKO WA BEI kuendelea kuwa mdogo licha ya gharama za mafuta

Nukta TV

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Hali ya uchumi Tanzania: Makadirio ya ukuaji wa uchumi Bara 6%, Zanzibar 6.6%

Nukta TV

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

BoT: Yatangaza ongezeko la riba ya Benki kuu hadi 6.25%

Nukta TV