Serikali yatoa tahadhari homa ya manjano

March 9, 2022 12:59 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Ugonjwa huo umelipotiwa nchini Kenya.
  • Yawataka wananchi kuchukua tahadhari ugonjwa huo usiingie nchini.
  • Yaimarisha upimaji mipakani na hospitali kuzuia maambukizi.

Dar es Salaam. Waziri wa Afya, Ummy  Mwalimu amewatahadharisha Watanzania kuchukua hatua dhidi ya ugonjwa wa Homa ya manjano ambao umeripotiwa kuwepo nchini Kenya ikiwemo kupata chanjo dhidi ya ugonjwa huo.

Ummy katika taarifa yake iliyotolewa leo Machi 9, 2022, amesema Serikali imepokea taarifa kutoka  Shirika la Afya Duniania (WHO) ya kuwepo kwa mlipuko wa ugonjwa huo nchini Kenya ambao unaweza kuingia nchini.

Kwa mujibu wa Ummy, ugonjwa huo tayari umegharimu maisha ya watu watatu huku watu 15 wakiwa na maambukizi nchini Kenya.

Kutokana na hali hiyo, amewataka Watanzania kuchukua hatua ya kuhakikisha ugonjwa huo hauingii Tanzania kwa sababu mpaka sasa hakuna viashiria vyovyote kuwa ugonjwa huo upo nchini.

“Hapa nchini taarifa ya kipindi cha miezi mitatu iliyopita katika mfumo wa ufuatiliaji wa magonjwa zinaonyesha kuwa hakuna taarifa zinazoashiria kuwepo kwa ugonjwa wa homa ya manjano, pia taarifa za ufuatiliaji wa tetesi za magonjwa haujaashiria kuwepo kwa ugonjwa huo,” amesema.

                         

Hatua ambayo inachukuliwa na Serikali kwa sasa ni kuboresha mifumo ya kutoa vyeti vya kielektroniki vya homa ya manjano mipakani ili kuzuia udanganyifu unaoweza kusababisha kusambaa kwa maambukizi.

“Tutaboresha mifumo ya kutoa vyeti vya kielektroniki vya homa ya manjano mipakani ili kuzuia udanganyifu unaoweza kufanywa na maafisa kuwapa vyeti watu ambao hawajachoma chanjo,” amesema Waziri Mwalimu.

Pamoja na tahadhari hiyo, Waziri Mwalimu ameziagiza hospitali zote za rufaa nchini kuwa na huduma za kupima na kutoa chanjo ya homa ya manjano kwa wasafiri na wenye uhitaji.


Soma zaidi:


Pia amewaagiza maafisa wa afya mipakani kuhakikisha wasafiri wanaoingia kutoka nchi zenye maambukizi wanakua na vyeti vya chanjo dhidi ya ugonjwa huo.

Dalili za ugonjwa wa homa ya manjano kama homa, kuumwa kichwa, maumivu ya misuli na mgongo, mwili kutetemeka, kupoteza hamu ya kula, kichefuchefu na kutapika.

Dalili nyngine ni pamoja na mwili kuwa wa njano pamoja na kutokwa na damu sehemu za wazi.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.