Magonjwa ya mfumo wa hewa yalivyowatesa Watanzania mwaka 2022-23

May 15, 2023 11:58 am · admin
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Watanzania wanatakiwa kuchukua tahadhari ya kujikinga na magonjwa yanayoathiri mfumo wa hewa mara baada ya Takwimu za Wizara ya Afya kubainisha kuwa ugonjwa huo umeathiri watu milioni 7.4 mwaka huu wa fedha.

Ugonjwa huo umeshika namba moja kati ya magonjwa 10 ya wagonjwa wa nje (OPD) yaliyoongoza kwa kuwaathiri Watanzania mwaka 2022/23.

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu aliyekuwa akisoma hotuba ya bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka 2023/24, Mei 12, 2023 bungeni jijini Dodoma aliwaambia wabunge kuwa maambukizi katika mfumo wa hewa ndio umeathiri watu wengi zaidi kati ya magonjwa 10 ya nje (OPD).

Ugonjwa huo ulishambulia watu milioni 7.4 sawa na asilimia 24 ya watu milioni 31.4 walioathirika na magonjwa hayo 10.

“Magonjwa yaliyoongoza katika kuwaathiri zaidi wananchi na kuwasababishia kwenda katika vituo vya huduma kupata matibabu ni maambukizi katika mfumo wa hewa asilimia 24, maambukizi ya njia ya mkojo asilimia 13, malaria (asilimia ),” amesema Ummy Mwalimu.

Magonjwa mengine ni Nimonia iliyoathiri watu milioni 1.3, kuhara chini ya siku 14 watu milioni 1.2, shinikizo la damu watu milioni 1.1 yakifuatiwa na magonjwa mengine ya mfumo wa mmeng’enyo , minyoo, vidonda vya tumbo na fangasi. 

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW