Serikali yamuhoji Nabii aliyedai kugundua dawa ya kutibu virusi vya Corona

February 14, 2020 6:29 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Imesema inataka athibitishe madai yake ya kuwa ana dawa ya kutibu ugonjwa huo.
  • Imesema akishindwa kuthibitisha atachukuliwa hatua kali za kisheria.
  • Mpaka sasa, Serikali imesema hakuna mgonjwa yeyote aliyegundulika kuwa na virusi hivyo nchini. 

Dar es Salaam. Serikali ya Tanzania imesema inamuhoji  mkazi wa mkoa wa Arusha, Mosses Mollel  anayejiita Nabii namba saba ili athibitishe madai yake kuwa ana uwezo wa kutibu virusi vya ugonjwa wa #Corona ambavyo mpaka sasa vimeua watu zaidi ya 1,300 ulimwenguni.

Hata hivyo, imewahakikishia Watanzania kuwa nchi bado iko salama na hakuna mgonjwa yeyote aliyeambukizwa virusi hivyo. 

“Kimsingi nimeiona hiyo taarifa ya huyo mtu  anayejiita Nabii Saba kuwa anayo dawa ya kutibu ugonjwa wa Corona, ila hapa kwetu Tanzania hatuna maambukizi yoyote ya ugonjwa huyo, tunachotaka huyo mtu  atuthibitishie uwezo wake wa kutibu huo ugonjwa wa Corona,” amesema Naibu Waziri wa Afya, Dk Faustine Ndugulile jana (Februari 13, 2020) mkoani Arusha. 

Amesema hadi sasa Serikali imetuma wataalamu wake kwenda kumsaka na kumhoji kama anavyo vibali vya kutoa huduma ya tiba na kujitangaza kuwa anatoa huduma ya kutibu ugonjwa huo  hatari ambao hadi sasa jumuiya za kimataifa zinahaha kusaka tiba ya ugonjwa huo.

“Tuepuke kutoa kauli ambazo zinakwenda kuchanganya jamii na endapo tutabaini mtu huyu hana sifa ambazo anasema kuwa nazo tutamchukulia hatua za kisheria,” amesema Dk Ndugulile ambaye pia ni Mbunge wa Kigamboni jijini Dar es Salaam. 


Soma zaidi: 


Nabii Namba Saba ambaye ni mkazi wa Ngaramtoni Wilayani Arumeru mkoani Arusha amekuwa akijitangaza kuwa anayo dawa ya kutibu ugonjwa huo wa virusi vya Corona na kuweka mawasiliano yake  kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo YouTube .

Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema mlipuko huo hadi Februari 13 ulikuwa umewaambikiza watu 46 997 kote duniani na kuwauwa zaidi ya 1,368 ambapo asilimia 99 ya visa vya ugonjwa huo vimetokea China. 

WHO kwa kushirikiana na wataalam wanaendelea na juhudi mbalimbali za kutafuta dawa ya ugonjwa huo ambao unasambaa kwa njia ya hewa na kushikana mikono na mgonjwa aliyeathirika. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV