Serikali kudhibiti mifuko ya plastiki kwa wageni wanaoingia Tanzania

May 16, 2019 7:30 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link

Uamuzi wa kupiga marufuku mifuko ya plastiki ulitangazwa bungeni  Aprili 9, 2019 na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ikiwa ni hatua ya kulinda mazingira na kuchagiza matumizi ya mifuko mbadala inayotengenezwa kwa teknolojia rahisi. Picha|Mtandao.


  • Hawataruhusiwa kuingia na mifuko ya plastiki ya aina yoyote ifikapo June 1 mwaka huu.
  • Serikali kuanzisha vituo maalum vya ukaguzi mipakani na kwenye viwanja vya ndege. 

Dar es Salaam. Serikali imewataka wageni wote wanaokusudia kuingia nchini kuanzia Juni 1 mwaka huu kuzingatia marufuku ya kutokubeba na kutumia mifuko ya plastiki ikiwa ni hatua ya kutunza mazingira na kuhakikisha nchi inakuwa safi wakati wote. 

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo (Mei 16, 2019) na Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, inaeleza kuwa aina zote za mifuko ya plastiki ya kubebea vitu bila kujali upana wake haitaruhusiwa kuingia, kusafirishwa, kutengenezwa, kuuzwa, kutunzwa, kusambazwa na kutumika Tanzania bara. 

Kutokana na marufuku hiyo, wageni wanaoingia nchini wanashauriwa kutokubeba mifuko ya plastiki katika mizigo yao ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza wakati wa ukaguzi. 

“Wageni wanaoingia Tanzania wanashauriwa kuepuka kubeba mifuko ya plastiki au vifungashio vya plastiki katika mabegi au mizigo ya mkononi kabla ya kutembelea Tanzania,” inasomeka sehemu ya taarifa hiyo. 

Ili kuhakikisha zoezi hilo linapata mafanikio, Serikali inakusudia kuanzisha dawati maalum katika vituo vya kuingilia wageni ikiwemo mipakani na viwanja vya ndege vitakavyotumika kukagua wageni wanaoingia na mifuko ya plastiki. 


Soma zaidi: 


Hata hivyo, taarifa hiyo imeweka wazi kuwa marufuku hiyo haitahusu mifuko au vifungashio vya plastiki vinavyotumika katika huduma za afya, bidhaa za viwandani, sekta ya ujenzi na kilimo. Pia, mifuko inayotumika kuhifadhia chakula, usafi na takataka haitahusika. 

Pia mifuko inayofungwa kwa zipu (ziploc bags) ambayo ni maalum kwa kubeba vipodozi itaruhusiwa kwa sababu inabaki katika umiliki wa wageni kwa sababu haitarajiwi kutupwa nchini. 

Serikali imesema haikusudii kuona marufuku hiyo inawaletea tabu wageni wanaoingia nchini bali ni hatua muhimu inazochukua kulinda mazingira na kuweka nchi katika hali ya usafi na kupendeza. 

“Serikali inatarajia kuwa, wageni watakubaliana na usumbufu mdogo unaoweza kujitokeza wakati utekelezaji wa marufuku ya matumizi ya mifuko ya plastiki,” inaeleza taarifa hiyo. 

Uamuzi wa kupiga marufuku mifuko ya plastiki ulitangazwa bungeni  Aprili 9, 2019 na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ikiwa ni hatua ya kulinda mazingira na kuchagiza matumizi ya mifuko mbadala inayotengenezwa kwa teknolojia rahisi. 

Ikiwa marufuku hiyo itaanza kutumika kama ilivyopangwa, Tanzania itaungana na nchi za Rwanda, Kenya pamoja na Zanzibar ambazo tayari zimezuia mifuko ya plastiki katika nchi zao. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
21 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
21 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
21 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Nukta TV

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Nukta TV

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

Nukta TV