Serikali kuanzisha mamlaka mpya ya Tiseza kuchochea uwekezaji 

February 13, 2025 3:43 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  • Itachukua nafasi ya Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na Mamlaka ya Ukanda Maalumu wa Uwekezaji Tanzania 

Dar es Salaam. Serikali ya Tanzania inakusudia kuanzisha Mamlaka mpya ya Uwekezaji na Maeneo Maalumu ya Kiuchumi Tanzania (Tiseza) ili kuchochea kasi ya uwekezaji mpya, kuuendeleza na kuusimamia vyema.

Mamlaka hiyo itaundwa kwa kuunganisha Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) pamoja na Mamlaka ya Ukanda Maalumu wa Uwekezaji Tanzania (EPZA), jambo linalotarajiwa kuongeza kasi ya uwekezaji kwa kupunguza urasimu.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Prof Kitila Mkumbo aliyekuwa akiwasilisha Muswada wa Sheria ya Uwekezaji na Maeneo Maalumu ya Kiuchumi wa 2024 bungeni jijini Dodoma amewaambia wabunge kuwa chimbuko la muswada huo ni kutekeleza uamuzi wa Serikali wa kuziunganisha taasisi hizo mbili.

Kitila amesema kuwa kuanzishwa kwa mamlaka hiyo mpya kutaboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kutoka ndani na nje ya nchi na kuchochea ukuaji wa uchumi.

Picha za matukio katika kikao cha kumi na tatu cha mkutano wa kumi na nane wa Bunge kilichofanyika leo. Picha/ Bunge la Tanzania/X.

“Serikali ya awamu ya sita ilipoingia madarakani, ilidhamiria kukuza uwekezaji na kuboresha mazingira ya biashara kama sehemu muhimu ya kuchochea ukuaji wa uchumi nchini,” amesema Prof Mkumbo.

Aidha, Prof Mkumbo alibainisha kuwa, mswada huo una malengo ya kuweka masharti ya uendelezaji wa uwekezaji Tanzania, kuweka masharti ya mazingira bora kwa wawekezaji, na kuweka mfumo wa kitaasisi kwa ajili ya uratibu, ulinzi na  uvutiaji uwekezaji.

Kwa mujibu wa Kitila muswada huo unapendekeza maboresho makubwa katika sekta ya uwekezaji, ikiwa ni pamoja na fursa na vivutio kwa wawekezaji wa ndani kwa kuweka vivutio mahsusi kwa wawekezaji wa ndani pekee.

Pia muswada huo ambao umeshapitishwa na Bunge unapendekeza kuanzishwa kwa benki ya ardhi ambayo itahusika na kutenga maeneo ya uwekezaji, huku watu binafsi na makampuni wakiruhusiwa kusajili ardhi zao kwa ajili ya uwekezaji.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge walichangia juu ya mswada huo akiwemo Haji Omary amebainisha kuwa njia zilizotumika kupendekeza mswada huo ni njia bora za ushirikishaji kwa kuangalia maeneo mazuri.

Kwa upande wa Mbunge wa Jimbo la Mwibara Charles Kajege ameshauri watumishi watakao kuwa kwenye mamlaka hiyo kuhakikisha kuwa wanakuwa mbele ya wakati ili kutambua vivutio na kujua namna ambavyo watapata wawekezaji.

Katika kikao cha leo Wabunge walipata fursa ya kuuliza Maswali ya Papo kwa Papo kwa Waziri Mkuu. Picha/Bunge la Tanzania

“Inabidi watumishi wa mamlaka hii wapate nafasi za kwenda kujifunza katika mamlaka ya nchi nyingine…hii itasaidia watumishi wetu kuwa mbele ya wakati. Mimi nashauri Serikali pamoja na mambo mengine ihakikishe kwamba watumishi wa mamlaka yetu hii wawe na uwezo wa kuongea lugha nyingi za kigeni,” ameeleza Kajege.

Licha ya kuunga mkono mswada huo Mbunge wa viti maalum kutoka mkoa wa Mwanza Mary Masanja amesisitiza kuwa suala la utoaji wa ardhi liwe na mchakato ya kuwafanya wazawa kulipwa fidia kwa wakati na kuwepo kwa mfumo mzuri kati ya wawekezaji wa ndani na wa nje.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
13 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
13 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
13 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

🔴LIVE: HII HAPA BAJETI KUU YA SERIKALI 2026/2027

Nukta TV

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Mashine za kukaushia rangi za kucha kutozwa ushuru kwa asilimia 10

Nukta TV

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Wazee wa 'kubet' hii inawahusu, 5% kutozwa kwenye dau la kamari

Nukta TV