SAUT yasitisha udahili kozi tano mwaka wa masomo 2025/26

July 22, 2025 3:27 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  • Kozi hizo ni pamoja na Sheria, Sosholojia pamoja na Mahusiano kwa Umma.

Dar es Salaam. Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino (SAUT) kimesitisha udahili wa kozi tano za shahada ya kwanza katika mwaka wa masomo 2025/26 ikiwemo za sosholojia (sociology) pamoja na falsafa.

Uamuzi huo umewekwa wazi siku chache tu tangu Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kusitisha udahili wa wanafunzi katika programu tisa za shahada ya kwanza za ualimu kwa mwaka wa masomo 2025/2026.

Afisa habari wa chuo cha SAUT Living Komu ameiambia Nukta Habari kuwa uamuzi huo umefikiwa mara baada ya Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) nchini kutoridhisha na uwiano kati ya walimu na wanafunzi wa kozi hio.

“Ambacho kimesababisha programu hizi zisidahili ni uwiano kati ya wanafunzi na walimu kwenye baadhi ya kozi, uwiano wa TCU nchini lazima uwe sawa yaani kwamba mwalimu mmoja afundishe wanafunzi 50,” ameeleza Komu.

Komu ameeleza kuwa kati ya kozi 14 zinazotolewa chuoni hapo, zilizozuiliwa ni pamoja Shahada ya kwanza ya Sheria, Shahada ya Sanaa katika Sosholojia, Shahada ya Falsafa Pamoja na Elimu, Shahada ya Utalii Usimamizi wa Huduma za Wageni pamoja na Shahada ya Mahusiano kwa Umma.

Hata hivyo, Komu amebainisha kuwa zuio la TCU huwa linatolewa katika muda husika wa masomo na iwapo chuo kikitimiza vigezo basi kozi hurejeshwa tena.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
21 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
21 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
21 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Nukta TV

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Nukta TV

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

Nukta TV