Sababu za vioo vya magari kuwa na madoa meusi

December 17, 2019 9:03 am · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  • Alama za madoa hayo hutumika kushIkilia kioo kisipate hitilafu ya kuanguka au kuvunjika.
  • Alama hizo zimechukua nafasi ya vishikizio vya chuma vilivyokuwa vinatumika awali.
  • Bado madereva wengi hawajui matumizi ya alama hizo. 

Dar es Salaam. Kama ni mmiliki wa gari au ni msafiri mzuri kwa kutumia magari binafsi, bila shaka umewahi kuona mwonekano fulani katika vioo vinavyozunguka gari lako ambao ni  alama za vidoti vidogo vidogo vyeusi katika ukingo wa vioo hivyo.

Alama hizo siyo za bahati mbaya. Zimewekwa kwenye magari mengi yanayotumika kipindi hiki cha ukuaji wa teknolojia ya kisasa. Kazi kubwa ya alama hizo kusaidia kushikilia kioo wakati wa kushusha na kupandisha ili kisiharibike au kuvunjika. 

Alama hizo kwa kawaida zimetengenezwa kwa rangi iliyochanganywa na gundi inayotumika maalum katika magari binafsi.

Teknolojia hiyo ya alama za vioo imechukua nafasi ya zamani ya vishikizio vyenye asili ya chuma ambavyo vilikuwa vinatumika kushikilia kioo.

Licha ya kufanya kazi ya ya kusaidia kioo kushikika vizuri, lakini pia husaidia kupunguza joto kwenye vioo hivyo, jambo linalosaidia kupunguza hatari ya vioo kuvunjika mara kwa mara ikilinganishwa na vishikizio vya chuma ambavyo pia havina muonekano mzuri. 


Zinazohusiana:


Hata hivyo,  ni madereva wachache wanafahamu maana ya alama hizo zinapokuwa katika kioo cha gari na baadhi yao wamefikia hatua hata ya kuzitoa, jambo lililosababisha kuvunjika kwa vioo vya magari yao.

Mmoja wa madereva taxi katika kituo cha Plam Beach jijini Dar es Salaam Danford Elias anasema amewahi kujaribu kuondoa alama hizo na kioo hakikudumu muda mrefu kikaachia. 

“Kuna mambo mengi tunafanya kwa kutokujua. Mimi nilidhani ni urembo ila mimeshabadilisha kioo cha gari yangu kwa kutoa alama hizo bila kujua umuhimu wake,” amesema.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV