Sababu baadhi ya bidhaa za chakula kutengwa Soko Kuu la Kariakoo
February 16, 2026 6:19 pm ·
Fatuma Hussein
- Ni pamoja na kuweka usawa wa mzunguko wa wateja katika sakafu zote.
Dar es Salaam. Wafanyabiashara wa mboga mboga katika Soko Kuu la Kariakoo walalamikia mpangilio wa bidhaa muhimu kutengwa katika sakafu tofauti, hali inayodaiwa kuwasumbua wateja na kupunguza mauzo.
Malalamiko hayo yanahusu bidhaa kama vitunguu, nyanya, karoti na pilipili hoho ambazo zimewekwa sakafu ya pili, wakati mboga nyingine zikiwa sakafu ya chini.
Katika mahojiano na Nukta TV, wafanyabiashara hao wanasema wateja wengi wanapendelea kukuta bidhaa zote muhimu katika eneo moja badala ya kuzunguka sakafu mbalimbali, hali inayowachosha wanunuzi na kusababisha wao kupoteza mapato kutokana na kupungua kwa mauzo.
Latest
4 hours ago
·
Kelvin Makwinya
Wafanyabiashara Kariakoo watii maagizo wahama barabarani
6 hours ago
·
Fatuma Hussein
Viwango vya kubadilisha fedha Tanzania Februari 17, 2026
24 hours ago
·
Goodluck Gustaph
Nini hutokea kichwani unapokunywa pombe?
5 days ago
·
Kelvin Makwinya
Rais Samia kushiriki mkutano AU, Tanzania ikimaliza muda wake Baraza la Amani