Ripoti: Madhara ya Corona yangepungua kama tungechukua tahadhari mapema

May 13, 2021 5:36 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa (UN) ya matarajio ya ukuaji wa uchumi. 
  • Yasema wananchi na viongozi kutozingatia maelekezo ya wataalam wa afya kumezidisha athari za ugonjwa huo. 

Ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa (UN) imeeleza kuwa madhara ambayo dunia imeyapata hasa ya kiuchumi yaliyotokana na janga la virusi vya corona yangeweza kuzuilika iwapo Serikali za nchi zingechukua hatua za haraka mara baada ya kuripotiwa kisa cha kwanza cha Covid-19. 

Ripoti hiyo ya hali na matarajio ya uchumi duniani (WESP) iliyotolewa Mei 11 mwaka huu imesema maamuzi yasiyofaa dhidi ya Corona yamesababisha vifo vya watu 3.3 duniani na kuvuruga uchumi wa dunia.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, kushindwa kwa serikali duniani kuweka mifumo thabiti na baadhi ya viongozi kupuuza kitisho cha janga la corona kulichangia kwa sehemu kubwa wananchi kutozingatia maelekezo ya wataalamu wa afya ya kujikinga na ugonjwa huo ikiwemo kuvaa barakoa. 


Soma zaidi: 


Hata hivyo, imesema kufuatia kusinyaa kwa uchumi kwa asilimia 3.6 mwaka 2020, uchumi wa dunia unatarajiwa kupanuka kwa asilimia 5.4 mwaka 2021 kutokana na hatua mbalimbali za dharura zilizochukuliwa ikiwemo utoaji wa chanjo.  

Ripoti hiyo imependekeza mfumo wa dunia wa kutoa tahadhari kufanyiwa mageuzi makubwa kwa lengo la kuepusha janga kama la Corona kutokea tena.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia azindua minara 758, aacha maagizo mazito juu ya mkongo wa taifa

Rais Samia azindua minara 758, aacha maagizo mazito juu ya mkongo wa taifa

Nukta TV

JAJI MKUU: Njia za asili ni mojawapo ya njia halali za utatuzi wa migogoro

JAJI MKUU: Njia za asili ni mojawapo ya njia halali za utatuzi wa migogoro

Nukta TV

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Nukta TV