Ripoti: Madhara ya Corona yangepungua kama tungechukua tahadhari mapema
- Ni ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa (UN) ya matarajio ya ukuaji wa uchumi.Â
- Yasema wananchi na viongozi kutozingatia maelekezo ya wataalam wa afya kumezidisha athari za ugonjwa huo.Â
Ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa (UN) imeeleza kuwa madhara ambayo dunia imeyapata hasa ya kiuchumi yaliyotokana na janga la virusi vya corona yangeweza kuzuilika iwapo Serikali za nchi zingechukua hatua za haraka mara baada ya kuripotiwa kisa cha kwanza cha Covid-19.Â
Ripoti hiyo ya hali na matarajio ya uchumi duniani (WESP) iliyotolewa Mei 11 mwaka huu imesema maamuzi yasiyofaa dhidi ya Corona yamesababisha vifo vya watu 3.3 duniani na kuvuruga uchumi wa dunia.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, kushindwa kwa serikali duniani kuweka mifumo thabiti na baadhi ya viongozi kupuuza kitisho cha janga la corona kulichangia kwa sehemu kubwa wananchi kutozingatia maelekezo ya wataalamu wa afya ya kujikinga na ugonjwa huo ikiwemo kuvaa barakoa.Â
Soma zaidi:Â
- Ugonjwa wa Corona unavyopukutisha mifuko ya wanunuzi Kariakoo
- Serikali yamuhoji Nabii aliyedai kugundua dawa ya kutibu virusi vya Corona
Hata hivyo, imesema kufuatia kusinyaa kwa uchumi kwa asilimia 3.6 mwaka 2020, uchumi wa dunia unatarajiwa kupanuka kwa asilimia 5.4 mwaka 2021 kutokana na hatua mbalimbali za dharura zilizochukuliwa ikiwemo utoaji wa chanjo. Â
Ripoti hiyo imependekeza mfumo wa dunia wa kutoa tahadhari kufanyiwa mageuzi makubwa kwa lengo la kuepusha janga kama la Corona kutokea tena.
Latest