Redio bado zipo zipo sana Tanzania

February 12, 2022 10:20 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Idadi ya vituo vya redio Tanzania imezidi kuongezeka kwa kasi baada ya vituo 17 kuanzishwa ndani ya mwaka mmoja.

Dar es Salaam. Wakati dunia ikiadhimisha Siku ya Redio kesho Februari 13, 2022, redio ni chombo muhimu ambacho Watanzania wana kitumia kupata habari zinazowawezesha kufanya maamuzi katika maisha yao ya kila siku.

Licha ya kuongezeka kwa changamoto za kifedha zinazoendelea kuvikabili vyombo mbalimbali vya habari duniani, idadi ya vituo vya redio Tanzania imezidi kuongezeka kwa kasi baada ya vituo 17 kuanzishwa ndani ya mwaka mmoja.

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inaeleza katika ripoti mpya ya mawasilino ya robo ya mwisho ya mwaka 2021 kuwa hadi Desemba mwaka jana kulikuwa na vituo 210 vya redio nchini kutoka vituo 193 mwaka 2020.

Uchambuzi wa mwenendo wa takwimu za vituo vya redio uliofanywa na Nukta (www.nukta.co.tz) unaonyesha kuwa vituo vingi vya redio vilizaliwa mwaka 2016 baada ya vituo 42 kuanzishwa ndani ya mwaka mmoja.

Hata hivyo, mwaka 2018 ndiyo mwaka ambao vituo vichache zaidi vilianzishwa ndani ya mwaka mmoja kutokana na kuongezeka kwa vituo viwili tu vya redio kutoka 156 mwaka 2017 hadi 158 mwaka 2018.

Hata hivyo, takwimu hizo hazihusishi vituo vya redio vya mtandaoni na haziweki bayana aina ya vituo hivyo katika makundi kama vya kijamii, kidini au kitaifa.

Redio ni moja ya aina ya vyombo vya habari vinavyowafikia watu wengi zaidi nchini kwa mujibu wa tafiti mbalimbali za hivi karibuni.

Ripoti ya utafiti wa Taasisi ya Repoa wa Afrobarometer wa mwaka 2017 inabainisha kuwa redio ndiyo chanzo maarufu cha habari miongoni mwa Watanzania baada ya matokeo kubainisha watu 45 kati 100 hupata habari kupitia redio kila siku.

Licha ya utafiti kueleza kuwa sehemu kubwa ya watu Tanzania hupata habari kutoka redioni, Kitabu cha ubora wa habari cha mwaka 2017 (Yearbook in Media Quality in Tanzania 2017: What do we know?) kinabainisha kuwa habari za redioni bado zina ubora hafifu.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV